WAKULIMA WA MWANI WAHIMIZWA KULIMA KILIMO CHA KISASA


                                                          NA FATMA HAMAD,PEMBA

 Wakulima wa mwani wametakiwa kulima kilimo cha kisasa ili waweze kuzalisha zao hilo kwa wingi.

 Ushauri huo umetolewa na Afisa Mazimgira kutoka idara ya mazimgira na Ofisi ya makamo wa kwanza wa Rais  Hassan Hamad Hassan wakati akizunumza na wanavikundi vya ulimaji wa mwani huko kilindi Chake chake  Pemba.

 Amesema Sera ya Serikali ya Uchumi wa buluu ni kuhakikisha inawainua wakulima wa mazao ya baharini ili waondokane na umaskini.

 Hivyo alisema ni wakati kwa Wakulima wa Mwani kuondokana na kilimo cha zamani, na badala yake walime kilimo cha kisasa (walime kwa ajili ya biashara) jambo ambalo litawawezesha kuvuna zao hilo kwa wingi na kujipatia  kipato.

 "Niwaombe Wakulima mbadilike msilime kimazoe, mlime kilimo cha kisasa na mlime Mwani kwa ajili ya biashara, msilime panatosha,"alisema.

 

Sheha wa Shehiya ya kilindi  Nassor Muhammed Khamis aliwataka wakulima hao waliopatiwa mafunzo kuyatumia mafunzo hayo ili waweze kulima kilimo chenye ubora ambacho kinaendana na Soko la Dunia.

 

Nao badhi ya washiriki hao wameishukuru Serikali kwa kuwapitia Elimu juu ya ulimaji wa mwani wa kisasa pamoja na vitendea kazi, huku wakiahidi kuongeza jitihada ya kuzalisha na kuboresha kilimo Chao. 

 Mafunzo hayo waliopatiwa wakulima wa mwani  wa kikundi cha Nyumba nyeupe na Dongoni Coperative ni utekelezaji wa mradi wa SAPPHIRE wenye Lengo la kusimamia mazingira ya pwani katika maeneo ya PECCA ambao unaendeshwa na Ofisi ya Makamo wa kwanza wa Rais pamoja na Idara ya Mazingira.








 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.