MASHEHA WATAKIWA KUTOA ELIMU KWA JAMII JUU UWEPO WA BARAZA LA KUMUWAKILISHA MTUMIAJI crc]

 





Masheha wa shehia mbali mbali kutoka wilaya ya Micheweni wametakiwa kuwa mabalozi wazuri  wa kuifikisha elimu juu ya kulijua na kulitumia baraza la kumuwakilisha mtumiaji wa huduma za maji na nishati katika shehia zao ili Wananchi waweze kufikisha kero zao katika baraza hilo.

Hayo yameelezwa na Kaimu katibu Tawala wilaya ya Micheweni Kai Shaame Kai wakati akifungua mafunzo ya siku moja juu ya kulijua Baraza la kumuwakilisha mtumiaji wa huduma za maji a Niashati kwa masheha wa wilaya hiyo huko Micheweni Mkoa wa kaskazini Pemba.

 Amesema Masheha wananafasi kubwa ya kuwafahamisha wanajamii juu ya matumizi ya huduma za maji na Nishati pamoja na kuwafahamisha uwepo wa baraza hilo kwa lengo la kufikisha changamoto zao .


Akizungumzia juu ya uwepo wa Baraza hilo katibu mtendaji wa baraza  la kumuakilisha mtumiaji wa huduma za maji na Nishati [CRC ] Hadia Abdurahman Othman amesema lengo la kuwanzishwa chombo hicho ni kuwatetea watumiaji wa huduma hizo  katika kutatua kero zao na kuzifanya huduma za maji na Nishati kuwa bora kwaZanzibar.

Amesema Serikali kwa kuwajali wananchi wake imeamua kwa makusudi kuanzisha chombo hicho ili kutetea malalamiko ya wananchi jambo ambalo litasaidia upatikanaji wa huduma za kijamii  kwa urahisi.

Amesema Vijiji vingi vimekua vikilalamikia  juu ya ukosefu wa huduma za maji safi pamoja na umeme, hivyo masheha mnajukumu kubwa la kushirikiana na CRC  ili kuhakikisha shehiya zenu zinapata huduma hizo.



Akiwasilisha mada juu ya haki na wajibu wa mtumiaji mtendaji kutoka baraza la kumuakilisha mtumiaji [ CRC] Khamis Ame Mnubi amesema lengo la mkutano huo kwa masheha ni kutoa elimu kwa jamii kufahamu kwamba, upatikanaji wa huduma hizo ni haki yao ya msingi, hivyo wasibaki kimya bali watoe malalamiko wakati wanapozikosa na kuona zinapatiwa ufumbuzi.


Wakitoa ufafanuzi wawakilishi kutoka shirika la Umeme na Mamlaka ya maji  wilaya ya micheweni   Ali Rajabu na Suleiman Salim Shajaki wamesema kwa sasa wamejipanga vyema ili kuona kero za wananchi zimeondoka.




 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.