MAULID KHAMIS KASSIM NI MFANYABIASHARA MLEMAVU AOMBA MSAADA KWA WASAMARIA WEMA ILI AKUZE BIASHARA YAKE


 Maulid Ali Kassim ambae ni Mlemavu wa viungo anaeishi Kijiji cha Wawi wilaya ya yake  chake  Mkoa wa Kusini Pemba aliyeamua kujishuhulisha na biashara ndogo ndogo kwa ajili ya kuondokana na  utegemezi na kujikwamua na umaskani wa kipato.

Maulid mwenye  familia ya  watoto watano anasema kuwa  aliamua kuanzisha biashara zake ndogo ndogo mara baada ya kumaliza masomo yake ya lazima ya kidato cha 2 katika Skuli ya Sekondari Wawi kwa kuanzia na biashara ya malai, juice na biskuti za watoto kwa mtaji wa shilingi elfu arobaini.

Kwa sasa Maulid anafanya biashara ya nguo za watoto huko Mjini Chake Chake  ambapo alianza na mtaji  wa shilingi laki mbili na hadi sasa  anasema mtaji wake unaweza kufika milioni moja.

Ameeleza kuwa licha ya ulemavu wake alionao aliamua kujiajiri ili aepukane na omba omba, na utegemezi kwa watu wengine, huku akijua kuwa yeye anahitaji kuwa na mahitaji kama binadamu wote ikiwemo kuwa na mke na watoto.

 ‘’Niliamua nijiajiri mwenyewe ili niepukane na kuomba jambo ambalo litaniepusha na udhalilishaji, Alieleza Maulid’’.

Maulid alisema  kutokana na biashara yake anaendesha familia yake mwenyewe, na anasomesha  watoto wake ambapo mtoto  wa mwanzo anasoma darasa la Tatu, wa pili anasoma darasa la kwanza katika Skuli  ya  Michakaini na watatu anasoma Chekechea Machomane.

‘’Naendesha familia yangu mwenyewe, si mtegemei mtu,  wala siombi, na watoto wangu wote wanasoma Shule pamoja na Madrasa, Alisema Maulid.’’

Hata hivyo ameleza kuwa familia yake iko pamoja nae haija mtenga, wanamshirikisha katika masuala mbali ya kifamilia yanapotokezea na pia husaidia baadhi ya mahitaji  ya nyumbani kwake.

Akitaja changamoto ambazo anakumbana nazo   ni kukosa fursa ya kupata mikopo isiyo na riba jambo ambalo linamkosesha kuendesha biashara zake ipasavo.

‘’Sjapata msaada wowote wala sjui wapi  pakwenda nikaweza kusaidiwa, Alisema Maulid.’’

Hivyo amesema endapo atapatiwa mkopo wa shilling Milioni mbili ana uwezo wa kuzifanyia biashara na kuzirejesha.

Aidha ameitaka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutoa punguzo maalum la ulipaji wa kodi za biashara kwa watu wenye ulemavu, jambo ambalo litawafanya waendeleze biashara zao.

‘’Kodi tunayolipa ni kubwa hatuiwezi kulingana na biashara zetu ni ndogo hivyo tunaiomba serikali ituangalie na sisi Walemavu’’,  Alisema Maulid.

Kwa upande mwengine aliwashauri watu wenye ulemavu wenzake ambao wanajiweza wafanye  kazi ili wasiwe wa tegemezi  katika  Jamii na kuweza kujipatia  riziki zao za halali.








Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.