RASIMU YA MAREKEBISHO YA SHERIA ZA MAFUTA NA GESI ASILIA YA ZANZIBAR ITAWEZA KUSAIDIA KUKUZA UCHUMI WA NCHI.

 

SALIM HAMAD,PEMBA

WADAU na Watendaji wa taasisi mbali mbali za Umma Kisiwani Pemba,wamesema iwapo rasimu ya marekebisho ya Sheria za mafuta na Gesi asilia ya Zanzibar itaweza kusadia kukuza maslahi ya Umma.

Wakizingumza katika mkutano wa kujadili rasimu ya marekebisho ya Sheri za mafuta na gesi Asilia ya mwaka 2016 uliofanyika Gombani Chake chake Pemba wamesema itasadia kutatua changamoto kwa baadhi ya vifungu ambavyo vilikuwa vinajitokeza hapoawali.

Akiwasilisha mada katika Mkutano huo Mwanasheria kutoka taasisiya ZPRA Omari Sururu Khalfani amefahamisha Vipengele vilivyofanyiwa marekebisho ikiwemo mkanganyiko watafsiri.

Alisema tayari kwenye maeneo hayo walibaini kuna mapungufu na kuweza kuyafanyia marekebisho kuona mapungufu hayo yanaondoka.

Afisa mdhamini Wizara ya Uchumi wa Bluu na Uvuvi Kisiwani Pemba,Dr Salum Mohd Hamza alisema lengo kuu la kuwakutanisha wadau mbali mbali ni kutafuta maoni juu ya marekebisho ya sheria za mafuta na gesi asilia.

‘’Tumefanya mkutano na wadau wa taasisi mbali mbali za umma ikiwa lengo ni kutafuta maoni ya wananchi juu ya rasimu ya marekebisho ya sheria za mafuta na gesi asilia na tukafanikiwa kupata michango yao’’alisema.

Alisema wadau waliweza kuikubali na kuchangia baadhi ya Vipengele ambavyo vinahitaji kufanyiwa maboresho zaidi kabla ya kupitishwa rasimu ya Sheria ya Mafuta na Gesi Visiwani Zanzibar.

.

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.