umasikini wapelekea Vilabu kushindwa kusaili na uhamisho wa wachezaji Kisiwani Pemba

 


SALIM HAMAD,PEMBA

UKATA wa Kifedha unaovikabili Vilabu vya Madaraja mbali mbali Kisiwani Pemba,umesababisha Dirisha la usajili na uhamisho wa wachezaji kusuasua kutokana na baadhi ya Vilabu kushindwa kujitokeza katika Ofisi za Shirikisho la Soka (ZFF) Kisiwani hapa.

Dirisha la Usajili na Uhamisho Visiwani Zanzibar limefunguliwa rasmi Septemba 21 ambapo litarajiwa kufungwa  Novemba 11.

Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi  Katib Msadizi wa Shirikisho la Soka Kisiwani Pemba,Khamisi Hamad Juma alisema Zoezi la Usajili na uhamisho limekuwa gumu msimu huu kutokana na baadhi ya Vilabu kushindwa kuchukua fomu.

Alisema moja ya sababu inayopelekea vilabu kutojitokeza kuchuka fomu za Usajili na wachezaji wanatka kuwasajili ni kutokana na ukata wa kifedha unaovikabili vilabu vya Pemba,jambo ambalo limepelekea zoezi hilo kusuasua.

Alisema hadi sasa timu zilizojitokeza kuchuwa fomu kwa upande wa Primia ni timu ya Machomane United ambayo imechukua fomu 7 na timu ya Yoso Boys imechukua fomu 5 na timu ya Dot mond imechukua fom 4 .

Alisema kwa upande wa Vilabu vya Daraja la kwanza kanda ya Pemba,ni timu ya Chipukizi fomu 10 New Ston Town fomu 6 Afrikana fomu 2 Mwenge fomu 3 Chake Chake Star fom 2 na Hardrock fomu 5 za ndani Zanzibar na Fomu 7 kutoka nje ya Zanzibar ambayo ndio timu pekee iliyochukuwa fomu nyingi kwa sasa.

‘’Dirisha la Uhamisho Visiwani Zanzibar limefungulia tokea September 21 na linatarajiwa kufungwa rasmi November 11 saa tisa alaasiri hivyo Vilabu vinaombwa kutumia kipindi hichi kwa kufanya mabadiliko kwenye Vikosi vyao’’alisema Khamisi.

Hata hivyo Katibu huyo ameviomba Vilabu kujitokeza kuitumia fursa hiyo ya usajili kuboresha timu za zao licha ya changamoto ya ukata wa kifedha unaovikabili Vilabu vya Pemba.


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.