WASAIDIZI WA SHERIA PEMBA WAPIWA MSASA

                                NA FATMA HAMAD,PEMBA

AFISA mdhamini Ofisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Halima  Khamis  Ali  amewataka Wasaidizi wa Sheria kuendelea kutoa Elimu kwa jamii kuhusu masuala mbali mbali ya kisheria ili waweze kuzifahamu sharia , Haki zao pamoja wajibu wao.

Mdhamini huyo ameyasema hao katika hafla ya ufungaji wa mafunzo ya siku tatu juu ya kujadili mambo mbali mbali ya kimaendeleo  kwa wasaidizi wa sharia yaliofanyika  Gombani Chake chake Pemba.

Alisema Wasaidizi wa Sheria wanadhima kubwa katika kuhakikisha jamii inapata uwelewa wa kutosha juu ya masuala mbali mbali ya kisheria pamoja na kufahamu haki zao stahiki.

‘’Ndugu zangu Wasaidizi wa Sheria nyinyi mnajukumu kubwa la kuhakikisha Jamii inazielewa Sheria, hivyo niwaombe tu muendelee kujitoa na kujituma ili kuona Wanachi wetu wanaishi kwa amani bila migogoro alieleza,’’.

Alisema Wananchi waliowengi hawana uwelewa juu ya masula ya kisheria, hivyo ni jukumu la Wasaidizi wa Sheria  kuhakikisha wanajitoa na kuipatia Elimu jamii ili iweze kuzifahamu Sheria, jambo ambalo litawafanya wawe na uthubutu wa kudai  na kutetea haki  zao pindi kukitokea uvunjifu wa haki hizao.


Akitoa neno la Shukurani katika hafla hiyo Msaidizi wa Sheria kutoka Jumuia ya Wasaidizi wa Sheria wilaya ya Mkoani Masoud Abdala alisema ni vyema kuwepo na utaratibu wa kuhakikisha wasaidizi wa Sheria kuwa ni miongoni mwa kamati za Masheha, ili kuweze kupatikana kwa mashirikiano ya kutosha baina ya Masheha na Wasaidizi wa Sheria, jambo ambalo litapelekea kuibua keronyingi ambazo zinawakwaza Wanachi na kuweza kuzitetea  na kuchukuliwa hatuwa kupitia kwa mamlaka husika itakayo lalamikiwa.


Nao baadhi ya Washiriki wa mafunzo hayo wameleza kuwa mafunzo  yamewajenga vyema, huku wakiahidi kuyafanyia kazi ili kuona Wananchi wanazifahamu sheria ambapo itasaidia kuepukana na dhulma ambazo wamekuwa wakifanyiwa badhi ya wanaJamii.


Mafunzo hayo ya siku tatu yenye lengo la kuwajengea uwezo Wasaidizi wa Sheria juu ya kuielimisha jamii masuala ya Sheria, yameandaliwa na Skuli ya Sheria pamoja na wizara ya Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora kupitia Idara ya Msaada wa kisheria chini ya ufadhili wa UNDP.



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.