WATOWA HUDUMA ZA MAMA MTOTO WATOWA YA MOYONI JUU YA HUDUMA YA M MAMA


                                    NA FATMA HAMAD, PEMBA

WAUGUZI  wanaotoa  huduma  za  Mama  na  Mtoto  wamesema  licha  ya  kuanzishwa  kwa  huduma  ya M mama  ambayo  imewekwa  kwa  lengo la  kutoa  usafiri  wa  haraka  wakati  ikitokezea  tatizo  kwa  mama  na  mtoto, bado  hauja  saidia  ipasavyo  katika  vituo  hivyo.

 Wakizunumza na wandishi wa habari wauguzi wa vituo vya Afya Wesha na Pujini walisema inapotokezea tatizo la mama na mtoto huduma za kuwahamishia Hospitali ya Wilaya inakua tatizo kwa vituo hivyo.

Amina  Ali Abdi ni Muguzi Mkunga kutoka kituo cha afya Wesha alisema mzazi anapopata tatizo akipiga simu kwa wahusika wa huduma ya M mama, kwa ajili ya kupata usafiri inakuwa ni shida,  jambo linalohatarisha maisha kwa Wazazi.

‘’Unaweza ukapiga simu tokea asubuhi kutaka usafiri kwa Uongozi wa huduma ya M mama kwa ajili ya kumuwahisha mgonjwa lakini haupatikani na hivyo unapopatikana haufiki kwa wakati, na kulazimika familia ya mzazi itowe gari yenyewe ndipo tuweze kumuhamishia Hospitali nyengine ’’alisema.

Kwa upande wake  Mkuu wa kituo hicho cha afya Wesha  Abdul nasir Hemed Said  alisema mfumo wa M mama bado haujakuwa na huduma rafiki kama ilivyotarajiwa.

Hivyo ameiomba Serikali kuboresha huduma hiyo ya M mama ili kuona kunaondosha matatizo yatokanayo na vifo vya mama na mtoto kama ilivyo dhamira ya Serikali.


Naye Muuguzi Mkunga kutoka kituo cha afya Pujini  Nasra Abdalla Juma amelalamikia juu ya kukosa mashirikiano kutoka kwa wahusika wa huduma ya (M mama) wakati wanapopata tatizo la mzazi na kutaka usafiri wa haraka  kwa ajili ya kumpeleka Hospitali ya wilaya ya Chake chake kwa ajili ya matibabu zaidi.


Afisa Mdhamini wiraza ya Afya Pemba Khamis Bilali Ali alisema wameshaweka mpango mkakati wa kuongeza madereva wa Ambalesi ambao watafanya kazi usiku na mchana katika kuwafikisha wagonjwa Hospitali kufuata huduma.

Mratibu wa huduma ya M mama Ofisi ya Pemba Maryam Ali Said aliwataka wahudumu wanaotoa huduma ya Afya ya mama na mtoto kuwatumia madereva ambao walisajiliwa na wizara ili kumuharakisha mazazi kunako husika na sio kusumbiria Ambalesi, jambo mabalo litaepusha vifo vya mama na mtoto.

‘’Tumesha waambia wakiona wamepata tatizo na wakipiga simu haipatikani wachukuwe madereva waliosajiliwa ili kumuhamisha mzazi kwa haraka, na wakimaliza watowe tarifa kwa wahusika wa M mama na kupatiwa malipo yao, wasikae nao tu wazazi,’’alieleza.

Alisema kwa sasa wameshaweka mpango mkakati wa kuhakikisha madereva wote waliosajiliwa na wizara wanapata malipo yao kwa wakati ili kuona wanafanya kazi masaa 24, jambo ambalo litaenda sambamba na dhamira ya Serikali ya kuhakikisha hakutokei vifo vya mama na mtoto vitokanavyo na uzazi.

Sera ya wizara ya Afya ya Zanzibar ya mwaka 1990 ni kuhakikisha inaimarisha huduma za afya ya uzazi ya mama na mtoto, ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi pamoja na vya watoto wachanga.

 Katika kipindi cha utekelezaji july 2022 hadi kufikia march 2023, wizara kupitia idara ya uendeshaji na utumishi inajukumu la kuhakikisha kuwa wizara inanyenzo ikiwa ni pamoja na rasili mali watu, fedha, majengo, usafiri na vitendea kazi.

 

 

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.