WAZIRI KADUARA ATOA MAGIZO KWA WIZARA YA KILIMO NA YA MAJI


                       NA FATMA HAMAD, PEMBA

WAZIRI wa Maji na Nishati Zanzibar  Shaib Hassan Kaduara  ameitaka wizara ya Kilimo kushirikiana na Wizara ya Maji kuhakikisha wanachimba Kisima katika eneyo la Chamanangwe pamoja na maeneo mengine, jambo ambalo litawasaidia wakulima kupata Maji na kuweza kuzalisha mazao kwa wingi.

Waziri huyo ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi pamoja na viongozi mbali mbali katika hafla ya  ufungaji wa siku ya Chakula duniani huko Chamanangwe  wilaya ya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba alisema Maji ni moja ya chanjo kikubwa kinachotegemewa na wakulima wengi kwa ajili ya uzalishaji wa mazao.

Alisema maji ndio msingi mkuu wa upatikanaji wa Chakula, hivyo ni wakati kwa wizara ya maji kuhakikisha wanasambaza maji katika maeneo mbali mbali na  wakulima waweze kuzalisha mazao mengi ili  kupatikana kwa chakula cha kutosha.

‘’Ni wakati kwa Mamlaka ya Maji pamoja na wizara ya  Kilimo kuchimba Kisima katika eneo la Chamanangwe na hata Vijijini kote ili wakulima waweze kulima mazao ambayo yatatusaidia katika maisha yetu,’’alisema.

Aidha aliwaomba Wananchi kujikita zaidi katika Sekta ya kilimo ili waweze kujiajiri, na kujipatia  chakula ambacho kitasaidia kuondokana na Njaa Kisiwani humo.


Akisoma Hotuba kwa niaba ya Mratibu wa Umoja wa Mataifa Nchini Tanzania  mwakilishi kutoka  Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO)  Stela Kiambi alisema maji ni chanzo kikubwa kinachosaidia kuondokana na njaa pamoja na umasikini Nchini.

Alieleza kuwa ukosefu wa maji unawadhibu watu zaidi ya Bilioni mbili pointi 4 Duniani kote,  ambapo asilimia 10 wanaishi katika Nchi zenye ukosefu mkubwa wa Maji.

‘’Wakulima wadogo hasa wanawake pamoja na vijana wako hatarini zaidi kukosa maji,’’ alisema.

Katibu mkuu wizara ya Kilimo maliasili na Mifugo Seif Shaban Mwinyi alisema kuwa bila ya kuwepo kwa huduma ya Maji hakuwezi kupatikana kwa maendeleo, hivyo ni wakati Serikali kuhakikisha inaimarisha huduma hiyo Vijijini kote ili kuona kunaondokana na upungufu mkubwa wa Chakula pamoja na matunda. 


Nae mkuu wa mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib alisema atahakikisha anaimarisha suala la Aamani na utulivu ili kuona Wanachi wanaendelea na shuhuli zao hizo za kimaendeleo bila ya tatizo lolote.

Maonesho hayo ya siku ya Chakula Duniani yaliendelea kwa muda wa siku 7 hapo katika viwanja vya Chamanangwe ambapo ujumbe wa mwaka huu unasema Maji ni uhai, Maji ni chakula hachwi mtu nyuma.



 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.