NA SALIM HAMAD,PEMBA
WANAFUNZI wa Skuli za Mwambe za Dkt. Samia Suluhu Hassan
Sekondari, Dk. Hussein Mwinyi Msingi na Mwambe Msingi wamehimizwa juu ya muhimu
ya kutoa taarifa pale wanapokubwa na changamoto mbali mbali zikiwemo za
viashiria vya vitendo vya kufanyiwa uzalilishaji wa kijinsia.
Wito huo umetolewa na
Mratibu wa Chama cha Waandishi Wanawake Tanzania, Zanzibar (Tamwa)Fat-hiya
Mussa Said wakati akiwasilisha mada juu ya Changamoto zinazowakabili watoto
katika mafunzo yaliyoandaliwa na Shirika la Save the Children na kuwajumuisha
wanafunzi wa Skuli hizo.
Alisema zipo
changamoto nyingi zinazowakumba watoto ikiwemo unyanyasaji wa kijinsia,
kimwili, kingono, kutekelezwa na nyengine nyingi lakini watoto hao wamekuwa
wakishindwa kuziripoti jambo ambalo husababisha wafanyaji kuendelea na vitendo
hivyo wakitambua kuwa hawaulizwi.
Alisema watoto hao
wanapaswa kuwaeleza wazazi wao, walimu, viongozi wa dini na watu wengine wa
karibu kila wanapohisi kuwa kuna viashiria vya kufanyiwa unyanyasaji ili kuweza
kuzuiwa visifanyike na wale ambao hubahatika kufanyiwa kwa hila au nguvu za
aina yoyote wasisite kutoa taarifa hizo katika wakati muafaka.
Alisema kuwa katika
eneo hilo la Mwambe yapo matukio kama ya ulawiti kwa watoto na watoto wenzao,
ubakaji, ndoa za umri mdogo lakini kutokana na kunyamaziwa na watoto
wanaofanyiwa huwa haziwezi kubainika hadi pale wanapoweza kubainika na
kulazimishwa kusema ndipo hueleza huku wakiwa wameshachelewa.
Kwa upande wake Afisa
Mradi Jumuishi katika Shirika la Msaada kwa watoto la Save the Children John
Maftah alisema kuwa kila mtoto anayo haki ya kulindwa na vitendo vya ujatili
ikiwemo kupigwa, kutelekezwa, kupakwa au kuozweshwa mume akiwa bado na umri
mdogo.
Alisema kuvujwa kwa
haki za watoto ni kinyume na haki za binadamu za juwakosesha haki zao za msingi
ambapo Save the Children imekuwa ikishirikiana na wadau mbali mbali katika
kuona haki za mtoto zinalindwa kwa mujibu wa sheria ya mtoto ya Zanzibar Sheria
namba 6 ya mwaka 2011.
Naye Afisa Takwimu
Katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Wilaya ya Mkoani Moh`d Abdalla
aliongeza kusema kuwa watoto wengi wa mwambe hufanyiwa vitendo vya
udhalilishaji lakini hushindwa kuripoti licha ya ofisi yake kupokea taarifa
hizo kila kukicha huku Mwambe ikiongoza kwa matukio hayo.
Akizungumzia mafunzo hayo
mwanafunzi Subira Khamis Juma wa Skuli ya Sekondari ya Dkt. Samia alisema
ukimwa wao ulitokana na kutokujua wapi na namna gani wanaweza kutoa taarifa za
udhalilishaji unapotokea kwao.
Ibra Ali Bakari
alikadhia kwa kusema kuwa kutokana na kupata elimu hiyo wataendelea
kuhamasishana wanafunzi kuona wanaripoti matukio hayo yanapofanyiwa wanafunzi
na watoto wengine wote na kutoa wito kwa wazazi kutopuuza pale wanapowapa
taarifa kama hizo.
Aidha wazazi na walezi
katika maeneo hayo ya mwambe wamepatiwa elimu juu ya kuwalinda watoto wao na
changamoto za udhalilishaji wa kijinsia kwa kufuatilia nyenendo zao.
Rehema Mjawiri Omar
kutoka dawati la polisi wilaya ya mkoani alisema kuwa suala la muhali limekuwa
likichangia kuongezeka kwa vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia kwani
anapotokea suala hilo jamii hukaa na kulimaliza kienyeji badala ya kuliripoti
kwa vyombo vya sheria kutokana na muhali.
Hakimu Dhamana
katika Wilaya ya Mkoani Suleiman Said Suleiman alisema kesi za udhalilishaji
zinazofikishwa mahakamani na kushindwa kutolewa hukumu kunasababishwa na
kukosekana kwa ushahidi kwa mashahidi waliotegemewa kutoa ushahidi hushindwa
kufika mahakamani badala ya kukaa vikao na jamii kulimaliza mitaani kwao.
Comments
Post a Comment