ALIANZIA UWAZIRI WA WANAWAKE NA WATOTOU WA SERIKALI YA WANAFUNZI NA SASA UKATIBU TAWALA
NA FATMA HAMAD,PEMBA ‘’Sitoisahau siku nilioteuliwa nafasi ya Ukatibu Tawala’’. Hayo ni maneno ya Bi Mkufu Faki Ali (51) ambae ni Katibu tawala wilaya ya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba Kwa hofu aliokua nayo mwanzoni nafasi hiyo hakuifurahia, kwani alihisi ni nafasi kubwa kwake. ‘’Watu wakipata uteuzi huwa wanafurahia, ila sikufichi mimi sikuile ya mwanzo nilishindwa hata kula nilikua nikilia,’’anasema. Aliteuliwa Octoba 2017 kipindi hicho alikua mfanya kazi wa Tume ya Uchaguzi wilaya Wete Kaskazini Pemba. Nafasi hiyo ilimuia vigumu, kwani ilikua bado ni mdogo, akiangalia anaowaongoza anaona wengine ni watu wanaomzidi na anaowaheshimu ‘’Nilipokua Chuoni nilikuwa Waziri wa Wanawake na watoto na niliiweza, hivyo nikajipa moyo na hiyi nitaiweza,’’alifahamisha. Mwana mama huyo aliezaliwa mwaka 1973, kijiji cha Utaani, kwasa anaishi Kizimbani wilaya ya Wete, Safari yake ya utumishi, ilianzia katika taaluma ya ...