Posts

Showing posts from August, 2026

ALIANZIA UWAZIRI WA WANAWAKE NA WATOTOU WA SERIKALI YA WANAFUNZI NA SASA UKATIBU TAWALA

Image
              NA FATMA HAMAD,PEMBA   ‘’Sitoisahau siku nilioteuliwa nafasi ya  Ukatibu Tawala’’. Hayo ni maneno ya Bi Mkufu Faki Ali (51) ambae ni Katibu tawala wilaya ya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba Kwa hofu aliokua  nayo mwanzoni nafasi hiyo hakuifurahia, kwani alihisi ni nafasi kubwa kwake. ‘’Watu wakipata uteuzi huwa wanafurahia, ila sikufichi  mimi sikuile ya  mwanzo nilishindwa hata kula nilikua nikilia,’’anasema. Aliteuliwa Octoba 2017 kipindi hicho alikua mfanya kazi wa Tume ya Uchaguzi  wilaya Wete Kaskazini Pemba. Nafasi hiyo ilimuia vigumu, kwani ilikua bado ni mdogo, akiangalia anaowaongoza anaona wengine ni watu wanaomzidi na anaowaheshimu ‘’Nilipokua Chuoni nilikuwa Waziri wa Wanawake na watoto na niliiweza, hivyo nikajipa moyo na hiyi nitaiweza,’’alifahamisha. Mwana mama huyo aliezaliwa mwaka 1973, kijiji cha Utaani, kwasa anaishi Kizimbani wilaya ya Wete, Safari yake ya utumishi, ilianzia katika taaluma ya ...