ALIANZIA UWAZIRI WA WANAWAKE NA WATOTOU WA SERIKALI YA WANAFUNZI NA SASA UKATIBU TAWALA

 

            NA FATMA HAMAD,PEMBA

 ‘’Sitoisahau siku nilioteuliwa nafasi ya  Ukatibu Tawala’’.

Hayo ni maneno ya Bi Mkufu Faki Ali (51) ambae ni Katibu tawala wilaya ya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba

Kwa hofu aliokua  nayo mwanzoni nafasi hiyo hakuifurahia, kwani alihisi ni nafasi kubwa kwake.

‘’Watu wakipata uteuzi huwa wanafurahia, ila sikufichi  mimi sikuile ya  mwanzo nilishindwa hata kula nilikua nikilia,’’anasema.

Aliteuliwa Octoba 2017 kipindi hicho alikua mfanya kazi wa Tume ya Uchaguzi  wilaya Wete Kaskazini Pemba.

Nafasi hiyo ilimuia vigumu, kwani ilikua bado ni mdogo, akiangalia anaowaongoza anaona wengine ni watu wanaomzidi na anaowaheshimu

‘’Nilipokua Chuoni nilikuwa Waziri wa Wanawake na watoto na niliiweza, hivyo nikajipa moyo na hiyi nitaiweza,’’alifahamisha.

Mwana mama huyo aliezaliwa mwaka 1973, kijiji cha Utaani, kwasa anaishi Kizimbani wilaya ya Wete, Safari yake ya utumishi, ilianzia katika taaluma ya uwalimu.

SAFARI YA KUELEKEA KWENYE UONGOZI

Mwaka 1980 alianza masomo katika  skuli ya Msingi Kizimbani,  na baada ya miaka saba, aliingia Utaani Sekondari kuendeleza na elimu yake.

 Mnamo mwaka 1990 alimaliza masomo yake ya darasa la 11 ingawa hakubahatika kuingia darasa la 12.

   Kufeli kwake hakukumfanya apoteze tumaini, alijipanga upya, alijiunga na Chuo cha Ufundi Dodeani Wingwi ili atimize ndoto zake.

 ‘’Hapo Ufundi nilianza darasa la tisa hadi la 12 nikafanya mtihani nikafaulu nikabahatika kuingia Fom iv skuli ya Fidel Castro iliyopoChakechake,’’ anafahamisha.

 Aliendelea kukata viatu akiisaka elimu kwa hali na mali, mwaka 1996 alijiunga rasmi na Chuo cha uwalimu Nkurumah, katika ngazi ya cheti.

 Alipoingia Chuoni hapo tu, alianza kujifunza majukumu ya Uongozi, kwani, alikua Waziri wa wanawake na watoto kwa kipindi chote alichokuwepo hapo.

 ‘’Nilikua sipendi kukaa nyumanyuma na ndio maana nikachaguliwa nafasi hiyo na niliitumikia kama inyotakikana,’’anasema.

 Mnamo mwaka 1998 alianza kuvuna matunda,  aliajiriwa na kufundisha katika skuli ya Jadida iliopo Wete Pemba.

 ‘’Nilipoanza kuonja matunda hayo utamu ulinichachukia, baada ya miaka nane, nilijiunga tena na Chuo cha Uwalimu cha Nkuruma katika ngazi ya Diploma na nikamaliza mwaka 2007,’’anasema.

 Hakutosheka na hapo kwavile alikua na ndoto za kufika mbali, mwaka 2008 alijiunga na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania katika ngazi ya Shahada ya kwanza.

 Ilipofika 2015 alijihisi hajafika sehemu anayoitaka, alijichukulia shahada ya pili ya Huduma za Jamii (MASTER OF SOCIAL WORK) katika Chuo kikuu Huria na kumaliza mwaka 2020.

 Baada ya kumaliza masomo yake, akiwa anaendelea na majukumu yake ua Uwalimu, alipata uhamisho kutoka skuli ya Jadida, na kupelekwa Limbani Wete.

 Hapo ndipo alipoanza kuonesha uwezo wake wa kufanya kazi kwa bidii, kwani ilikua ndo mwalimu mdogo kuliko wote.

 ‘’Iilikua wananituma mara tupikie chai, tusafishie, tukoshee vyombo, nilikua ninawatumikia kwa furaha na kwa tabasamu,’’anasimulia.

 Yote hayo hakua akichoka, alifanya kazi yake kwa imani na hilo lilimjengea heshima na kufikia mwaka  2007 alipelekwa Tume ya Uchaguzi na kuwa Msaidizi Afisa Uandikishaji wa wilaya,’’anaeleza.

 ‘’Kumbe vile nilivyonikifanyiwa ilikua mtihani, nashukuru niliufaulu, na mwaka 2017 serikli iliniamini, ikaniteua nafasi ya Ukatibu Tawala wilaya ya Wete.

 Mwanzoni baada ya kupata nafasi hiyo aliogopa, kwani wilaya ya Wete, ilikua na watu ambao walikua na misimamo na mihemko ya kisiasa.

 ‘’Ingawa nilikua na hofu, ila nilijenga uthubutu, nimeitumikia vyema nafasi hii wananchi wananikubali wananiamini,’anasema.

 Hatimae ulemsemo unaosema ‘nyotanjema huonekana alfajiri; kwa Bi Mkufu umesadifu, kwani nafasi hile alioanza kuitumikia akiwa chuoni, imekua ufunguzi wa yeye kuendelea kuwa kiongozi.

 Tokea apate nafasi hiyo ameshakaa na wakuu wa wilaya zaidi ya watatu, amekua akifanyakazi zake kwa uangalifu, hajawahi kukwaruzana nao.

 ANAYOJIVUNIA 

Moja analojivunia katika uongozi wake ni kuimarisha uhusiano wa kijamii, kuishi kwa upendo na mshikamano, na kushiriki kwa pamoja katika shughuli za maendeleo.

 ‘’Mji wa Wete ulikua ni mithili ya moto wa kifuu, ila nimeutuliza, wananchi wanikubali na tunaishi kwa amani, kwa upendo,’’anasimulia.

 Mbali na hilo, amekua akiwasadia mitaji wananchi wanyonge, wafanye shughuli za kiuchumi wajipatie kipato waendeshe familia zao.

 ‘’Akinijia mwananchi nimsaidie sioni tabu, natoa pesa zangu, nampatia mtaji afanye biashara

ajipatie kipato aendeshe maisha yake,’anaeleza.

 Sambamba na nafasi hiyo alishawahi kuteuliwa kuwa Mshauri wa Kamati za shehia, Mlezi wa Madrasa mbalimbali za Wete.

 CHANGAMOTO KATIKA KAZI

 Maranyingi vikwazo vinavyomkwaza katika uongozi wake ni nidharau nakuitwa maneno mabaya na baadhi ya watu wasiopenda maendeleo ya wanawake.

 ‘‘Wapo baadhi ya watu hunidharau na hunipa maneno yanye kunikatisha tamaa,’’anasema.

 WATU WANAOMFAHAMU

Salma Saleh Hamad Afisa Ustawi wa Jamii wilaya ya Wete, uongozi Katibu Tawala wao Bi Mkufu umewakomboa kwani wanapata fursa mbalimbali ikiwemo likizo.

 ‘’Tulikua stahiki zetu tunazikosa, likizo, na ‘Overtime’ tulikua hatupati hapo kabla ya uongozi wake Bi Mkufu,’’anasema.

 Mohamed Hamad Ali mlinzi wa Ofisi ya mkuu wa Wilaya, anasema uongozi wa Bi Mkufu ni wa mfano, kwani anawajali na amekua na tabia ya kuwaweka vikao akisikiliza kero zao.

 ‘’Kama kuna nafasi ya Mkuu wa Mkoa, basi tunaomba apewe,  mama huyu anajitahidi, ni muadilifu

anaongoza kwa hekima,’’anafahamisha.

 MASHEHA

 Omar Khamis Othman Sheha wa Kiungoni, anasema Mkufu ni kiongozi anaefanya kazi kwa bidi,  anafuatia wafanyakazi wake, simbaguzi, anajali utu.

 ‘’Mamayetu huyu ni mchapa kazi, hapendi kukaa tu Ofisini anafuatilia kazi zetu, anapenda umoja na wala hana ubaguzi na yoyote,’’anasema.

 Ramia Said Rashid sheha wa Bopwe, anasema yeye Bi Mkufu anamuona anafaa kwa kiongozi, kwani anajiamini, na anapambana kila hali, katika kutatua shida za wananchi.

 Mkuu wa wilaya ya Wete Abdalla Rashid Ali anasema Mkufu ni kiongozi imara, mchapa kazi na anajali kazi yake pamoja na watendaji.

‘’Huyu  mwanamama yuko vizuri,ni mfano tosha kwa viongozi wanawake, nafurahi hata mimi nilipokwenda alinipokea vizur,’’anasema.

Hakujifanya kama ni kiongozi wa serikali tu, bali anabeba nafasi ya umama katika jamii yake, akisikia kuna jambo Fulani analifuatilia hadi anahakikisha amelipatia ufumbuzi.

Namsifia hasa kwani amechukua nyayo za kiongozi wetu mamayetu Samia Suluhu Hassan, amekua habagui, hachagui anajali maendeleo kwa wote.

WANAHARAKATI 

 Afisa program kutoka Chama cha Wandishi wa Habari wanawake Tanzani ( TAMWA ZANZ) Khairat Ali anasema, uwepo wa viongozi wanawake ni hatua muhimu katika nchi.

 ‘’Uwakilishi wa wanawake katika maamuzi unasaidia kubadilisha sera, ingawa bado kunachangamoto za kimfumo na mitazamo tofauti kuhusu kasi ya mabadiliko hayo,’’anasema.

 MIKATABA

 Ripoti na Mitazamo ya Mitandao ya kijami inasema maranyingi wanawake huleta mabadiliko wanapopewa nafasi, kwani hutumia busara, ushawishi, kutatua migogoro na kuleta utulivu katika jamii zao.

Ilani ya Uchaguzi na serikali za mitaa  ya mwaka 2019 na  Uchaguzi Mkuu 2020  inalenga  serikali kuu iliyoko madarakani na ile itakayoshika madaraka na taasisi zake, ina wajibu wa kuhakikisha kuwa uwanja wa ushindani wa kisiasa ni huru na wa salama kwa makundi yote hususani wanawake.

 Mkataba wa kimataifa wa haki za kiraia na haki za kisiasa ya mwaka 1976 kifungu cha 25, kinaeleza kila raia ana haki ya kupiga kura na kuchaguliwa katika uchaguzi wa kweli, wa haki na wa mara kwa mara, uliofanywa kwa kura ya siri.

Hata Katiba ya Zanzibar ya 1984, ambayo ndo sharia mama, kupitia kifungu chake cha  21(1) nacho kinatambua haki ya kila raia kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi bila ubaguzi.

Dira ya Maendeleo ya 2050 inasema Usalama na usawa wa kijinsia ni nguzo kuu katika mabadiliko ya kijamii na utekelezaji wa sera za nchi.

Kisiwa cha Pemba inazowilaya nne, ikiwa Makatibu Tawala  wilaya ni sawa kati ya wanaume na wanake.

 MWISHO

 

Comments

Popular posts from this blog

WANDISHI WA HABARI ANDIKENI HABARI ZA UCHAMBUZI

HOFU YA UDHALILISHAJI MTANDAONI INAVYOWANYAMAZISHA WANAWAKE

UROHO WA MALI KWA WANAUME UNAVYONYIMA WANAWAKE ARDHI