MASHEHA WATAKIWA KUTOA ELIMU KWA JAMII KUFAHAMU ULIPAJI WA KODI YA MAJENGO

 

Uploading: 31292625 of 51030747 bytes uploaded.


                      NA FATMA HAMAD,PEMBA

MKURUGENZI wa Bodi ya mapato (ZRA] kisiwani Pemba  Jmal Hassan Jamal amewataka Masheha kuielimisha Jamii  kufahamu umuhimu wa kulipa kodi ili  waweze kulipa kodi jambo ambalo litaipatia Nchi maendeleo.

Mkurugenzi huo ameyasema hayo wakati akizungumza na Masheha pamoja na viongozi mbali mbali wa Serikali wa mkoa wa Kaskazini Pemba katika mkutano wa utoaji wa uelewa wa kodi ya majengo huko baraza la Wawakilishi Wete mkoa wa Kaskazini Pemba amesema ulipaji wa kodi ni moja ya chanzo kitakachoipatia Nchi kupiga hatua kimaendeleo.

Alisema masheha wana nafasi kubwa katika jamii, hivyo ni jukumu lenu kuwaelimisha wananchi ili kuhakikisha wanatekeleza juku lao la ulipaji wa kodi.

‘’Ndugu zangu masheha ni wajibu wenu kutoa elimu kwa jamii ili kuona wanatekeleza wajibu wa Serikali wa ulipaji wa Kodi,’’alisema.

Aidha  kwa upande mwengine alifahamisha kuwa  miongoni mwa majengo yatakayolipiwa kodi ni majumba  ya Ghorofa pamoja na majengo yanayotumika kwa ajili ya biashara, na sio majengo mengine ya kawaida.

‘’Kodi ya majengo haiwahusu Wananchi bali  itawahusu wenye nyumba za ghorofa tu, ikiwa yanatumika kwa biashara na hata kwa ajli ya makaazi,’’ alifahamisha.

Alisema majengo ya ghorofa yanayotumika kwa ajili ya makazi yatalipiwa Shilingi 10,000/= kwa mwaka kwa kila jengo moja,,.

Majengo ya biashara yenye ghorofa yatalipiwa Shiling 50,000/=, ambapo majengo mengine yasio ya biashara yatalipa 50,000/=.

Na majengo ya Hoteli za ghorofa zitalipa kulingana na hadhi ya majengo hayo.

Akifungua mkutano huo Mkuu wa mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib amemtaka Kamishna wa [ZRA] Zanzibar kuendelea kutoa elimu kwa watu mbali mbali kuhusu sualala kodi ya majengo  ili kuona Wananchi wamepata uelewa wa kutosha juu ya suala hilo. 

 

 

 

 

 

 

 


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.