WADAU WA HAKI ZA BINADAMU WATAKIWA KUONGEZA NGUVU KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA VITENDO VYA UDHALILISHAJI

                             NA SALIM HAMAD,PEMBA

MKURUGENZI  wa Mashtaka Zanzibar, Mgeni Jailan Jecha amesema  bado kuna juhudi ndogo zinazochukuliwa na wadau katika  mapambano  ya vitendo vya udhalilishaji  kwani   baadhi yao huzisuluhisha kesi hizo kienyeji  jambo ambalo husababisha  kesi hizo  kupotea bila ya  kuchukuliwa hatua za kisheria.

 

Alisema bado wapo baadhi ya watendaji hao  hupatanisha kesi hizo Kiuenyeji ili zisiende mahakamani jambo ambalo linakwamisha juhudi za mapambano ya kesi hizo na kusababisha kuendelea kujitokeza Vitendo hivyo.

 

Mkurugenzi aliyasema  hayo  wakati akifungua  mafunzo elekezi juu ya kuchunguza na kuendesha kesi zinazohusiana na  udhalilishaji wa kijinsia  kwa wadau wa mapambano juu ya kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji ikiwa ni pamoja na waendesha mashtaka, madaktari,Maafisa na polisi  huko katika  ukumbi wa Makonyo Chake chake.

Alisema sababu nyengine ni jamii kutotilia maanani katika mapambano ya vitendo vya udhalilishaji kwa kuona kuwa jukumu la mapambano hayo ni la Serikali pekee ama Polisi na mahakama.

 

Alifahamisha kuwa ili vitendo vya  udhalilishaji  viweze kuondoka ni vyema Kwa taasisi zinazoshughulikia  kesi jinai ziweze kupambana kwa pamoja  huku  wakiondoa  ukakasi wa aina zote katika kufuatilia kesi hizo.

 

'’Mapambano haya ili yaweze kufanikiwa lazima yawepo mashirikiano ya pamoja kati ya taasisi husika na jamii Kwa kukataa ushawishi wowote unaorejesha nyuma ikiwemo rushwa muhali"alisema.


Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar, Mwanamkaa Abdurahman Mohammed alisema lengo la mafunzo hayo ni  kuondosha changamoto zinazojitokeza mahakamani ikiwa ni pamoja na uchunguzi  wa madaktari  na utowaji wa ushahidi mambo ambayo yanarudisha nyuma uendeshaji wa kesi hizo.

 

Alieleza  kuwa madaktari wana haja ya kujuwa ule utaratibu mzima ikiwemo kutowa ushahidi Mahakamani hivyo ni lazima kupata mafunzo hayo ili kuoondosha malalamiko yasiyo ya lazima.

 

Mapema Ofisa Mdhamini wizara ya Nchi Afisi Rais   Katiba ,Sheria Utumishi wa Umma na Utawala Bora,Halima  Khamis Ali alisema ni lazima kuondokana na vikwazo vinavyokwamisha keshi za udhalilishaji ikiwemo kutowa ushahidi wa kweli mahakamani ili haki uweze kupatikana .

 

Alieleza kuwa ili taifa liweze kuwa imara na lenye ubora lazima vyombo vinavyosimamia haki visiwe ndio kikwazo kinachokwamisha kesi hizo na badala yake viwe na ushirikiano na kuweka mikakati ili nguvu za mapambano ziweze kufanikiwa.

 

‘’Taasisi hizi za Mahkama Madaktari na Polisi Mmekuwa mkilalamikiwa sana na jamii kwa kutokuwa na uadilifu na kuondosha Imani kwa wananchi hivyo ni lazima mubadilike haki itendeke na asionewe mtu’’alisema.

 

Alisema Wadau hao kama watashirikiana ipasavyo Pamoja na wananchi vitendo hivyo vitawza kupungua kwa kiasi kikubwa hapa nchini na kurejesha imani kwa wananchi.

 

Akitowa mada ya namna ya kumfanyia uchunguzi muhanga wa kesi ya udhalilishaji Mkurugenzi tiba kutoka wizara ya afya Dk. Msafiri Ladislaus Marijani alisema jukumu la daktari ni kumpa matibabu muhanga ili aweze kendelea na Maisha pamoja na ukusanyaji wa ushahidi utakaosaidia mahakamani.

 

Alielekeza madaktari  wanapompokea muhanga wa udhalilishaji hakuna haja ya kuweka vikwazo na kupelekea  kupoteza ushahidi badala yake wafanye majukumu yao kama sheria inavyoelekeza.

 

‘’Madaktari na wao wanafasi kubwa katika kupambana na kesi hizo kwa kutoa Ushahidi halali pale wanapofanya uchunguzi wa kitaalamu kutambua mtuhumiwa wa vitendo hivyo ‘’alisema.






 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.