KATIBU MKUU CUF AACHA UJUMBE KWA VIONGOZI WENZAKE

 

                                      NA FATMA HAMAD PEMBA.

 Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF Hamad Massoud Hamad amewataka viongozi wenzake wa vyama vya siasa nchini kuyaenzi na kuyalinda  maridhiano  ya Zanzinbar  ili kuwafanya watu wote kuwa kitu kimoja.

Katibu huyo ametoa wito huo wakati akizungumza na wapenzi na wafuasi wa chama cha CUF  katika mkutano wake wa mwanzo tokea kuondolewa kwa zuio la mikutano ya hadhara na Rais  wa Jamuhuri ya Muungano  Samia Suluhu Hassan huko wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Alisema kazi walioifanya viongozi wa Zanzibar  akiwemo marehemu maalimu Seif Sharif pamoja na rais mwinyi la kufanya mazungumzo na kuanzisha maridhiano ni jambo kubwa, hivyo niwajibu viongozi kuyaendelenza na kuyatunza maridhiano hayo yaendelee kudumu hapa Nchini.

''Tumekua tukishuhudia kunapomalizika kwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar  katika vijiji vyetu hujitokeza migogoro mbalimbali ikiwemo kususiana, hivyo basi  Niwasihi viongozi wenzangu tuyaheshimu na tuyatunze maridhiano ili kunusuru migongano hiyo'' alisema katibu mkuu.

 Aidha Katibu huyo  aliwataka viongozi wenzake  wa vyama vya siasa kufanya siasa  za kistaarabu jambo ambalo litaepusha kujitokeza kwa vurugu  baina ya wafuasi wa  vyama tofauti kwenye mikutano yao watakaoifanya.

Kwa upande mwengine mheshimiwa Hamad alisema kitendo cha Rais Samia Suluhu Hassan cha kuruhusu shughuli  za mikutano ya hadhara ya kisiasa ni jambo la busara na ni jambo la kushukuriwa.

 Akitoa Salamu za wanawake wa  Pemba kwenye mkutano huo  Bi Fatma  Mabrouk amewataka wanachama  wanawake kushirikiana katika kukiimarisha  chama chao wakitambua kuwa CUF ndo ile ile yenye kujali haki na usawa kwa  watu wote.

Mapema  Naibu Katibu Mkuu wa CUF  Zanzibar  Mbarouk  Seif aliwashukuru  wanachama wote waliokuwa nje ya chama hicho na kuamua kurudi ili kuweza kushirikiana na wengine kukiimarisha chama chao.

Katika mkutano huo jumla ya wanachama  513  wa  wilaya  ya Micheweni  kutoka  chama  cha  ACT  Wazalendo  walichukua  kadi  za  chama  cha CUF.



 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.