WANDISHI WA HABARI WAPEWA MBINU ZA KUANDIKA HABARI ZA UDHALILISHAJI.

 

               NA FATMA HAMAD,

Wandishi wa habari wametakiwa kufuata madili na miko ya  uwandishi wa habari wakati wanapoandika na kuripoti habari zao, ili kuepusha migongano isiyo ya lazima.

Akizungumza na wandishi wa vyombo mbali mbali vya habari katika mafunzo ya kuwajengea uwezo jinsi ya  kuandika na  kuripoti  habari za udhalilishaji, Afisa mkuu wa mawasiliano na uchechemuzi kutoka chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Zanzibar Safia  Ngalafi, huko mkanjuni Chake Chake Pemba.

Alisema kwa mujibu wa  utafiti  wa kihabari  uliofanywa  na Tamwa  ili kuona jinsi gani  wandishi wa habari wanaripoti habari za udhalilishaji, imeonekana kuwa,  bado wandisi   hawajakuwa na uwelewa wa kutosha juu ya kuandika na kuripoti habari za udhalilishaji.

‘’ Tulifanya utafiti  kwa  kuangalia habari zinazoripotiwa na wandishi wa habari  kupitia Gazeti la Zanzibar leo, Nipashe, Habari leo,  Assalam fm, Furaha, pamoja na soio media.’’ Alisema bi safia.

Alisema bado wandishi wa habari wanahitaji kuendelezwa kielimu ili kuona wanandika habari zenye mashiko na maslahi kwa Taifa na Jamii.

Aidha aliwataka wandishi wa habari kufanya ufuatiliaji  wa stori zao wanazoziandika ili jamii ifahamu ni kwa namna gani  haki imetendeka.


Mapema mkufunzi kutoka chuo cha uwandishi wa habari [Suza] Aiman duwe amewataka wandishi wa habari kujikita zaid kuandika habari za uchunguzi, ambazo zitaleta maendeleo na mabadiloko katika jamii.


‘’Wandishi wa habari nyinyi mnadhima kubwa, hivyo endapo mtazitumia vizuri kalamu zenu  na kuondokana na woga, mnaweza mkawa chanzo kikubwa cha kuipeleka Nchi kupiga hatua kimaendeleo,’’ alieleza mkufunzi.

Nao wandishi waliopata mafunzo hayo walisema mafunzo hayo yatawasaidia kuandika habari zenye kuleta mabadiliko ndani ya jamii



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.