ZAFELA YAWA MSAADA KWA WATOTO WA KIKE WALIOACHA SHULE
NA FATMA
HAMAD,
Mkurugenzi
wa Jumuia ya Wanasheria wanawake Zanzibar
Zafela Jamila Mahmo
Mkurugenzi
huyo aliyasema hayo katika mkutano wa kuutambulisha mradi wa Malala,
utakaoendeshwa na Zafela visiwani Zanzibar kwa muda wa mwaka mmoja, kikao hicho
kilichowajumuisha asasi mbali mbali za kirai kisiwani Pemba.
Alisema katika
utafiti wao walioufanya waligundua kuwa ,kuna wimbi kubwa la watoto wa kike wamekuwa wakikatisha masomo yao kutokana na sababu mbali mbali,
ikiwemo kuolewa, kupata mimba za utotoni Pamoja na kufanyishwa kazi za nyumbani.
Alisema
wamekuwa wakipokea kesi nyingi za Watoto wa kike, kuda haki zao, aidha waliolewa
au waliojihusisha na mahusiano, ambao ukiwangalia umri wao unapaswa wawe
wako shuleni na wanaendelea na masomo yao.
‘’Tumeamua
kuleta mradi huu wa Malala kwa ajili ya
kumuezesha na kumsaidia mtoto wa kike
ili aweze kurudi shule na kumaliza masomo yake angalau hadi darasa la kumi na mbili,’’alisema
mkurugenzi.
Alifahamisha
kuwa mrahidi huo umelenga kuwafikia jumla ya Watoto 3000 kwa Unguja na Pemba, hiyo amezitaka asasi za
kiraia kuweka mashirikiano makubwa na
jumuia ya Zafela ili kuona mradi huo umefikia malengo.
Aidha kwa
upande mwengine mkurugenzi aliwataka
wanajamii kukaa karibu na Watoto wao na kuwasikiliza matatizo yao, ili wawe na
uthubutu wa kueleza changamoto zinazowatokezea katika harakati zao za kimasomo.
‘’Inawezekana
mtoto anaacha Shule kutokana na vikwazo tu vinavyo mkwaza aidha njiani au
shuleni, hiyo tujenge urafiki na Watoto wetu ili tuwanusuru na kadhia kama hizo,’’
alifahamisha mkurugenzi.
Mapema
msimamizi wa mradi huo Hairun Abass Rajab kutoka chama cha wanansheria wanawake Zanzibar [Zafela] Alieleza kuwa hadi
sasa bado zipo familia ambazo hazimpi fursa mtoto wa kike kupata haki yake ya
elimu kuanzia Msingi hadi Vyuo vikuu.
Alifahamisha kuwa lengo la mradi huo
nikuwasaidia Watoto walioacha Shule, na waliokatika mazingira magumu, ili
kuhakikisha wanapata elimu na kufikia ndoto zao.
Akichangia
katika mkutano huo mwanaharakati wa kulinda na kutetea haki za wanawake na Watoto kutoka wilaya ya Mkoani
Sada Moh’d Othman alisema ni vyema
kuweko na mkakati Madhubuti ya kuwaekea usimamizi wa hali ya juu wanafunzi
hao wakati watakapo rudi shuleni ili kunusuru vitendo viovu na waendelee na
masomo yao.
‘’Kuna Watoto
waliokaa nje kwa muda mrefu, na tayari walisha athirika na ulevi, ulawiti, ubakaji,
hivyo ni vyema tuwe makini nao, wakati tunapowarejesha shuleni, ili wasije
wakambukiza na wengine,’’alifahamisha mwanaharakati.
Nao washiriki
Ali moh’d Ali na Salim Said walisema ili kumaliza vitendo viovu katika jamii, ni lazima kila mmoja kwa nafasi
yake kuchukua jitihada za makusudi,
jambo ambalo litasaidia kupata kizazi chenye
madili mema.
Comments
Post a Comment