WANDISHI WAPEWA NENO

 


                                   NA FATMA HAMAD PEMBA.

 Wandishi wa habari  wametakiwa kutoa elimu kwa jamii ili  kufahamu  umuhimu wa afya ya uzazi.

Wito huo umetolewa na Afisa mdhamini wizara ya afya wakati akifunga  Mafunzo ya Siku tatu yanayo husu  afya ya Uzazi kwa wandishi wa habari huko katika ukumbi wa Chama cha Wandishi wa habari Wanawake Tanzania [TAMWA] Chake chake Pemba.

 Alisema imeonekana  bado jamii haina uwelewa wa kutosha  kuhusu afya ya uzazi,jambo ambalo linachangia  kukosa afya bora ya mama na mtoto.

‘’Ndugu zangu nyinyi wandishi wa habari ndio kioo kwa jamii, hivyo tunaomba mtusaidie kuielimisha jamii jambo ambalo litaepusha Vifo vitokanavyo vya uzazi,’’ alisema mdhamin bilali.

Aidha  aliiasa jamii kuacha tabia ya kuwaozesha  waume mabinti zao ambao hawajafikia umri wa miaka 18, kwani kutawaepusha na matatizo mbali mbali yatokanayo   na uzazi.

‘’Siku hizi kuna matatizo mengi jamani yatokanayo na uzazi, hivyo wazazi tuacheni tamaa ili tuwakinge watoto wetu,’’ alifahamisha mdhamin.  

Mapema  Afisa Miradi na Tathmini kutoka Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Ofisi ya Pemba, Mohammed Khatib Mohamed amesema mafunzo hayo yameletwa ili  kuwajengea uwezo  waandishi wa Habari ili kuielimisha jamii kuhusu masuala ya afya ya uzazi.

 Akiwasilisha mada katika mafunzo hayo mkufunzi  kutoka kitengo   Afya Dr Rahila Salim Omar amewashauri wananchi kutumia uzazi wa mpango katika kuimarisha afya zao.

 Nae  Mkufunzi wa mafunzo hayo  Ali  Mbarouk  Omar aliwataka  wanajamii kufika hospitali, kupima afya zao  na kupatiwa matibabu pindi watakapo gundulika na matatizo.

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.