UFAHAMU UZAZI WA MPANGO



                                                 NA FATMA HAMAD PEMBA

Wananchi kisiwani Pemba wameshauriwa  kutumia njia salama ya uzazi wa mpango hali ambayo itasaidia kuimarisha afya ya mama na mtoto.

 Ushauri huo umetolewa na mtaalamu wa masuala ya Afya ya uzazi  Rahila Salim Omar kwa wandishi wa habari kisiwani Pemba alisema zipo njia kadhaa za kupanga uzazi ambazo zote ni salama.

Alisema miongoni mwa  njia hizo  ni zile za kisayansi pamoja  na za kisasa   ambapo  hazina madhara yoyote.

Alisema miongoni mwa njia  hizo ni kama vile kitanzi kwa mama ambaye hajajifungua sana, sindano,vipandikizi,vidonge ambazo zote ni salama na   hutolewa kulingana na afya ya mama.

''Sio kweli kwamba ukipanga uzazi unapata matatizo tusidanganyane, kitalamu hakuna hilo njia zote zipo salama, alifahamisha docta Rahila''


kwa upande wake Sheikh Mohamed Nassor  Abdala kutoka jumuia ya maimau Pemba [JUMAZA]  Alisema Uislamu  hujakataza  uzazi wa mpango.

''Kisheria mtoto anatakiwa anyonye miaka miwili, ndipo mama abebe ujauzito,'' ili kuimarisha afya ya mama na mtoto,  "alifahamisha sheikh Nassor.

Aidha alifahamisha kuwa   njia  za kufunga uzazi zipo kwa wanawake na wanaume sio kwa wanawake tu, hivyo ni vyema wanaume nawao kuzitumia njia hizo.


 Kwa upande wao washiriki wa mafunzo hayo  walisema  wanashukuru  kupata  nafasi     ya kupatiwa mafunzo hayo,  hivyo  watahakikisha wanatoa ushirikiano katika kutoa elimu hio  ndani ya jamii.



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.