DC MICHEWENI APIGA VITA UNYANYAPAA DHIDI YA WATOTO WENYE ULEMAVU

 


NA FATMA HAMAD -- PEMBA.

Wazazi   na   walezi   wenye  watoto  wenye  ulemavu  wametakiwa  kuwapeleka   Skuli pamoja na madrasa  ili nawao  waweze kujipatia haki yao  ya elimu kama watoto wengine.

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi  kwa njia ya simu alisema bado wapo wazazi wanatabia ya kuwaficha watoto wenye ulemavu na badalake kuwakosesha haki zao.

‘’Niwaombe wazazi waache tabia ya kuwafungia ndani watoto wenye ulemavu kwani  nawao  ni binadamu kama wengine wanahitaji kupata haki zote stahiki, ’’alisema mkuu wa Wilaya.

Alieleza wapo wazazi katika jamii  wanapozaa watoto wenye ulemavu  wamekuwa wakiwanyanyapaa na kuhisi kama ni mkosi ndani ya familia yao, jambo ambalo haileti picha nzuri kwa mwenyewe mwenye ulemavu na hata kwa Mwenyezi Mungu.

Alifahamisha watoto wenye ulemavu waliowengi wanapenda kusoma na mara nyingi Mungu huwajaalia kipaji, hivyo ni budi wapatiwe fursa  mbali mbali ili waweze kutimiza malengo yao waliojiwekea.

‘’Tusiwatenge tuwapeni fursa  watoto wetu wenye ulemau ili nawao wawemo katika Sekta mbali mbali jamani, tutakwenda kuulizwa kesho mbele ya Allah(S,W)’’ alieleza mkuu wa wilaya.

Mapema sheha wa shehia ya Shumba ya vyamboni Time Said Omar alisema wanachukuwa jitihada mbali mbali ya kuwaelimisha jamii kuhakikisha wanawalinda na kuwapatia matunzo watoto wenye ulemavu.

Aidha aliwataka wananchi kutoa taarifa wakati watakamuona mtu mwenye ulemavu yoyote ananyanyapaliwa ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yake.

Nae mama mzazi  wa Abdala Hussein Rashid mwenye ulemavu wa viungo  Bi Time Kombo Juma  mkaazi wa Kwale gongo  alisema  licha ya ulemavu wake alionao mtoto wake  lakini hakumbagua alimpeleka madrasa, skuli na sasa ni mwanafunzi wa darasa la kumi katika skuli ya Sekondari kinyasini wilaya ya wete kaskazini Pemba.

Hivyo aliwataka wazazi  wenzake wenye watoto wenye ulemau wasikate tamaa waige mfano wake, wawasomeshe na wawapatie fursa mbali mbali ambazo zitaleta maendeleo kwao kwani nawao wanauwezo wa kufanya kazi.

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu cha 12[1] kinasema ‘’Watu wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayohaki bila ya ubaqguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria.


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.