WANAFUNZI MASKULINI WAPEWA NENO.
Wanafunzi wametakiwa
kuwa mstari wa mbele kutoa tarifa
kwa walimu au wazazi wao wakati
watakapoona viashiria vya udhalilishaji katika maeneo yao.
Wito huo
umetolewa na Msaidizi wa Sheria kutoka Jumuiya ya wasaidizi wa Sheria Wilaya ya
Micheweni Said Salum Khamis alipokuwa akitoa
elimu juu ya mapambano dhidi ya ukatili na udhalilishaji watoto huko skuli ya Sizini
ikiwa ni shamra shamra ya madhimisho ya siku ya mtoto wa afrika.
Alisema vitendo vya udhalilisha vinafanyika katika
mazingira ya jamii hivyo wakati umefika kwa wanafunzi kuondosha muhali bali watoe tarifa pale wanapoona vitendo vya udhalilishaji ili
viweze kuchukuliwa hatua za kisheria.
‘’Sasaivi
udhalilishaji unafanyika kila pahala hivyo msiogope toeni tarifa msiogope’’
alisema Said Salum.
Nae kwa upande wake afisa jinsia na watoto wilaya ya micheweni Bizume Haji
Zume amesema lengo la kutoa elimu hiyo
ni kufikisha ujumbe kwa wanafunzi juu ya kuisoma katiba ya Nchi ili waweze kuzitambua na kuzifahamu haki
zao za msingi wanazostahiki kuzipata
katika maisha yao.
Utoaji wa
elimu hiyo dhidi ya ya ukatili wa watoto ikiwa ni shamra shamra ya
madhimisho ya siku ya mtoto wa afrika ni ushirikiano wa Jumuia za wasaidizi wa
sheria, Chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania [TAMWA] na Kituo cha
huduma za sheria Zanzibar.
Comments
Post a Comment