WANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUZISOMA SHERIA
Wandishi wa
habari wametakiwa kuzisoma na kuzifahamu sheria mbali mbali ili waweze kuandika habari zenye ukweli ambazo zitaleta tija kwa jamii.
Ushauri huo
umetolewa na Mkuu wa wilaya ya Mkoani
Khatibu Juma Mjaja wakati akizungumza na wandishi wa habari katika mafunzo ya
kujadili sheria ya habari huko gombani Chake chake Pemba.
Amesema
wandishi wa habari ni wadau wakubwa ambao mnaweza kuiletea nchi mabadiliko
hivyo ni muhimu kuzifahamu kanuni na
sheria ambazo zitawaongoza kuandika
habari zenu kwa kuzingatia madili.
‘’Nyinyi
wandishi wa habari ni wadau muhimu katika Nchi
hivyo ni lazima muzisome sheria ili muweze kuwa wadilifu katika kazi
zenu’’ amesema Mkuu wa wilaya.
Katibu
mtendaji kutoka baraza la habari Tanzania [MCT] Kajubi Mukajanga amesema
kutokuzifahamu sheria sio kinga ya kutokuadhibiwa wakati unapoivunja, hivyo ni lazima musome sheria ili
muepuke kuandika habari zenye kusababisha migogoro.
‘’Msipo
zifahamu sheria mtandika habari ambazo
zitaleta migongano’’ amesema katibu
mtendaji.
Kwa upande
wake mwenyekiti wa baraza la habari
Tanzania [MCT] upande wa Zanzibar Shifaa Said Hassan amesema endapo wandishi wa
habari watazifahamu sheria pamoja na
vifungu vya Katiba kutawawezesha
kuibua habari zenye kuaminika na zenye kuifanya nchi kupiga hatua kimaendeleo.
Kwa upande
wake Ofisa mdahamini wizara ya habari vijana na Michezo Mfamau Lali mfamau amesema wandishi wa habari wasiandike habari kwa
mazoea, hivyo basi wakati umefika kubadilika
ili waendane na soko la Dunia.
Comments
Post a Comment