WANAOHARIBU USHAHIDI WAONYWA

 


NA FATMA HAMAD PEMBA.

Serikali ya mkoa wa Kusini pemba imesema  haitomvumilia  mtendaji yoyote  atakaebainika  anashiriki kuharibu ushahidi wa kesi ya udhalilishaji  kwa makusudi ili kesi hiyo isiendelee mahakamani.

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Masoud katika madhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika  huko Gombani Chake  chake Pemba.

Amesema  wapo baadhi ya watendaji  wakiwemo Madaktari hawataki kwenda mahakamani kutoa ushahidi hivyo  hatutokubali tutawachukulia hatua kali za kisheria  watakao kataa  kutoa ushahidi.

‘’Wapo madaktari ambao  mnawafanyia uchunguzi  wanaodhalilishwa  hamtaki kwenda kutoa ushahidi, lakini nimeshaliagiza jeshi la Polisi liwaweke ndani madaktari watakao kataa’’alisema mkuu wa Mko

Amesema  vitendo vya udhalilishaji vimeshakua tishio kwa jamii hivyo kama  watu watakataa kutoa ushahidi hakuna kesi itakaopata hatia  na badalayake tutaendelea kuibebesha  mzigo wa lawama mahakama  kwamba haitendi haki.


Mapema Ofisa mdhamini wizara ya Elimu na mafunzo ya Amali Pemba Muhamed  Nassor  Salim  amesema  bado  Jamii  yenyewe haijakua  tayari kupiga vita vitendo vya udhalilishaji.

‘’Sheria zetu ziko makini, watendaji wetu wako makini lakini jamii bado haijakua na sauti ya pamoja ya kusema sasa udhalilishaji basi’’ alisema Afisa mdhamini Elimu.


Akisoma katika maadhimisho hayo  mratibu  wa kituo cha huduma za sheria Zanzibar ofisi ya Pemba Safia Saleh Sultani amesema licha ya juhudi zinazochukuliwa na wadau mbali mbali kutoa elimum juu


Jumla ya  matukio  130  ya udhalilishaji yameripotiwa kuanzia Jane  mwaka  hadi March  mwaka  huu  katika mkoa  wa  Kusini Pemba.

 





 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.