TAMWA YAIBUA KASORO SHERIA ZA KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI




 

                                           13/2/2023.

NA FATMA HAMAD PEMBA

KATIKA  kupiga   vita suala la  udhalilishaji  wa  kijinsia, Serikali imeweka mikakati  mbali  mbali,  ikiwemo kufanya  marekebisho  ya  sheria, ambazo  zinahusu  masuala  ya  udhalilishaji  wa  kijinsia, ili  kuona  jamii  inaondokana  nalo.

Lakini  licha  ya  marekebisho  hayo  bado   vipo  vifungu  kadhaa  vya sheria, ambavyo vinaonekana  bado  vina mapungufu  na vinaleta ukakasi  juu ya uendeshwaji na utolewaji wa hukumu  kwa kesi za udhalilishaliji  katika vyombo vya sheria.

 WANAJAMII.                                                                

Kombo Ali Hamad mwanajamii kutoka wilaya ya Wete, amesema mtu yoyote atakae mnajisi mtu mwenye ulemavu asipewa dhamana kifuatwe kifungu cha 151 [1] cha sheria 7 ya 2018 sheria ya Mwenendo wa makossa ya Jina, kwani  wenye ulemavu na wao ni bidamu  na linathirika zaid  kundi hilo .

‘’ Mimi kwa maoni yangu nashauri icho kifungu  kinachozungumzia atakae mnajisi mgonjwa wa akili apewe dhamana, kifutwe kwani hakiwatendei haki watu wenye ulemavu,’’ alisema Kombo  Ali Hamad.

Watu wate wafuate sheria bila shuruti, hivyo yoyote atakaemdhalilisha mtu mwenye mlemavu wa akili, achukuliwe hatua na kupewa adhabu kwa mujibu wa sheria invyoelekeza.

Akashauri kuwa, asiachiliwe kwa sababu tu isionekanwe kama aliyemfanyia hana akili, mtazidi kuwapa nafasi ya kuwadhalisha.

Hidaya Mjaka Ali mwenye ulemavu wa viungo mkaazi wa shehia ya Vitongoji, amesema kwa sasa kifungu hicho kinachosema atakae mnajisi mlemavu wa akili apewe dhamana, hakifai.

Anasema, kwani anapokuwa nje anaweza akafanya chochot  ili aweze kuharibu ushahidi, hivyo ni vyema nae asipewa dhamana.

‘’Mimi kifungu hicho nakiona hakiko sawa, naomba kifutwe kabisa  hakifai, kwani licha ya kuwa ni mlemavu wa akili, lakini ni vyema kw amtuhumiwa awekwe ndani, mpaka utakapomalizika kwa ushahidi na ikithibitka hajafanya atatolewa,’’anasema.

Mara nyingi kesi za watu wenye ulemavu  zinapotokezea huishia njiani na hizo sheria zikiwa na mapungufu watu wanazidi kupata chaka la kujifichia wakazidi kuwadhalilisha watu wenye ulemavu.

MZAZI WA MTOTO MWENYE ULEMAU ALIEDHALILISHWA

Mimi mwakajana mtoto wangu mwenye ulemau wa akili na  matamshi  alibakwa na kupewa ujauzito, nikaenda kwa sheha na kesi akaifikisha kituo cha  Polisi Konde.

Mama huyu mkaazi wa Tumbe  hakuona   tabu  alisema atasimama mpaka haki ya mwanangu ipatikane nikaenda polisi siku ya kwanza nikambiwa niende siku nyengine.

Ilipofika siku niliopangiwa simu alikwenda  na mwanangu  akaitwa akatoa ushahidi wote,  ila kwa kweli  kwa mazingira niliyoyaona alikata tamaa  na kujua kuwa kesi  ya  mtoto wake haifiki popote.

 ‘’Mwisho wa siku kesi  ilifutwa katika kituo cha Polisi Konde mtuhumiwa yuko anaendelea na shughuli zake mtaani bila ya wasi wasi wala hofu,’’ alieleza mama huyo.

ALIEFANIKIWA KESI YAKE BAADA YA MDOGO WAKE KUDHALILISHWA

Mimi mdogo wangu  mwenye ulemavu wa akili,  mara baada ya kunajisiwa na Nuhu Kombo mkaazi wa Kijichame, niliipeleka kesi kituo cha polisi Micheweni, akaambiwa asubiri wanaendelea na upelelezi.

Anasema baada ya kumaliliza upelelezi wao, aliitwa kituoni na muathirika na kuanza kuchukuliwa maelezo.

‘’Sikukata tamaa niliendelea kuifuatilia kesi hiyo na kisha ilifikishwa mahakamani na sasa mtuhumiwa yuko Chuo cha Mafunzo akitukimia miaka saba (7).

WANAHARAKATI

Wanaharakati wa kupambana na masuala ya udhalilishaji, wamekuwa wakizipigia kelele sheria ambazo zinaonekana na mapungufu yanayopelekea uzoroteshwaji na ukosekanaji wa haki za wathirika wa vitendo vya udhalilishaji.

Fathiya Mussa Said kutoka TAMWA- Pemba amesema suala la kupewa dhamana kwa mtu atakae mnajisi mwenye ulemavu wa akili, ni tatizo na  ipo haja  ya kutokupewa dhamana.

‘’Tunaomba kifuatwe kifungu cha 151 [1] cha sheria 7/ 2018 na kifungu cha 116 cha sheria 6 /2018  kirekebishwe isiwe sababu ya kupewa dhamana  kwa sababu tu, amemfanyiwa mtu mwenye ulemavu wa akili,  tukifanya hivyo  tutaendelelea kuwadhalilisha na kuwakosesha haki zao.

JUMUIA YA WATU WENYE ULEMAVU WA AKILI [ZAPDD]

Khalfan Amour Mohamed ni Mratib wa Jumuia kwa ajili ya ya watu wenye ulemavu Zanzibar ‘ZAPDD’ kisiwani Pemba, anasema kuwa  ni vyema sheria ingetoa tafsiri halisi ya neono  la kunajisi, ili kujua nikupi huko, vyenginevyo  kiingizwe kwenye kifungu cha 151 cha sheria 7/2018 sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai.

 ‘’Tunataka tufahamu kifungu hicho  cha 116 cha sheria  namba 6/ 2018   sheria ya  Mwenendo wa Makosa ya Jinai,  jee kinawahusu watu wenye ulemavu  wa kili tu,   kwani hawa  wao si binadamu  hawana haki kwenye taifa hili,’’alihoji.

Sisi wadau wa watu wenye ulemavu tunataka kifungu cha 116 kifutwe kabisa, kwani kinaleta utofauti wa watu wenye ulemavu wa akili na wasio na ulemavu, tunataka kosa hilo liingizwe kwenye kifungu cha 151 kinachozungumzia dhamana.

 Hakimu wa mahakama maalumu ya kupamba na makosa ya udhalilishaji mkoa wa Kusini Pemba, Muumin Ali Juma amesema kesi za watu wenye ulemavu bado ni  changamoto kubwa, na mara nyingi hufutwa kutokana na kukosa ushahidi.

‘’Ukosefu wa wakalimani ni kikwazo kikubwa, kinachopelekea kesi nyingi za watu wenye ulemavu kushindwa kupatatiwa,’’ alisema hakimu Muumin.

  Kifungu cha (151) [1] cha sheria namba 7 ya mwaka 2018  cha  sheria  ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai,   sheria  ya  Zanziba  kimeorodhesha  makosa  ambayo hayana  dhamana,  ikiwa ni kubaka, kuingilia kinyume na maumbile, kumuingilia maharimu, kubaka kwa kikundi, kumnajisi mtoto wa kiume.

Lakini kosa la kumnajisI mtu mwenye ulemavu wa akili lililopo kifungu cha 116 cha sheria namba 6 ya mwaka 2018, kosa hili lina dhamana,

sheria hiyo imeonekana na kasoro  hivyo wadau   pamoja  na  anaharakati  mbali mbali  wa  kutetea masuala ya udhalilishaji  wakitaka kifutwe.

Tunataka kuwepo na sheria moja  tu  ambayo  itajumuisha makosa yote ya udhalilishaji badala ya kuepo na sheria tofauti tofauti kwenye kosa moja.

KATIBA YA ZANZIBAR.

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu cha 12 [1] kinasema watu wote  ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki bila ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawambele ya sheria, ikiwa katiba inasema hivyo, lakini bado watu wenye ulemavu wanaona  wanabaguliwa  juu ya  kifungu cha 116 cha sheria 6 / 2018 mtu akimnajisi mwenye ulemavu wa akili anapewa dhamana, lakini kifungu cha (151) [1] cha sheria namba 7 ya mwaka 2018  cha  sheria  ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai,   sheria  ya  Zanziba kinasema kuwa akinajisiwa mwenye akili zake timamu hapewi dhamana.

























 


                  

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.