UKOSEFU WA WALIMU MJUMUISHI UNAVYOATHIRI NDOTO ZA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU PEMBA
NA FATMA
HAMAD, PEMBA
‘’Namshukuru
nimefaulu mtihani wangu wa darasa la
kumi na leo nipo darasani na jumuika na wenzangu, kuchota
elimu hapa skuli ya sekondari Kinyasini,’’anasema mwanafunzi.
Hayo ni maneno ya mwanafunzi Hussein Abdalla Rashid mwenye ulemavu mchanganyiko mkaazi wa Kwale
gongo wilaya ya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba.
Abdalla ni mwanafunzi ambae anaisaka elimu katika mazingira magumu,
kwani anakotoka kijiji cha mbali na kwenye mabonde na milima.
‘’Ninatoka kjiji cha mbali ambapo ni kilo mita 10, kutoka nyumbani
kwetu hadi skuli, ila sijali kwani ndoto
yangu ni kuwa fundi wa umeme,’’ alisema Abdala.
CHANGA
MOTO ZA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU
Abdalla Husein Rashid amesema kuwa anatamani siku moja awe
fundi mkubwa wa
umeme, lakini bado wanakilio
kwenye Skuli zao hakuna walimu
wa kufundisha wanafunzi wenye
ulemavu.
Amesema kitendo cha wanafunzi
wenye ulemavu kuchanganywa darasa moja na wasio na ulemavu huku wakiwa hawana mwalimu wa kuwasaidia ni kikwazo kwa wanafunzi
wenye ulemavu.
‘’Mfumo wa elimu mjumuishi wa kutuchanganya darasa moja sisi wenye
ulemavu na wasio na ulemavu bado hauja tutendea haki kwani hatuna walimu wa
kutufundisha,’’ alisema.
Alisema kwa kweli hakua na tamaa ya kufalu darasa la kumi kwa sababu
toka anze darasa la kwanza, hadi kufikia hapo hajapatapo mwalimu hata siku moja
wa kumsaidia.
‘’Mimi nangalia tu ubaoni kinachoandikwa ndio naweka kichwani si fahamu chochote mwalimu
anachofundisha ila tu mungu na
rehema zake amenijalia nimefaulu’’.
Hivyo wamemuomba rais wao mpendwa kukiona na kukifanyia kazi kilio chao na kuwawekea mazingira rafiki ili nawao
watimize ndoto zao.
ya sekondari Utaani Wete Pemba mwenye ulemavu wa viungo ameeleza kuwa anandoto ya kuwa Mhandisi majengo.
Amesema
ili aweze kutimiza ndoto yake
hiyo ni vyema serikali
ikawajengea skuli yao malumu na kuwawekea miundombinu ya kutosha,
kama vile walimu wa lugha
za amala, vitabu vya kufundishia pamoja na
kuwapatia misaada ya viti mwendo.
‘’Licha ya ulemavu wangu lakini nasoma kwa bidi, kwani nina hamu ya kuwa ‘injinia’ mkuu wa majengo, namuomba rais wetu atuangalie kwa jicho la huruma na sisi tunayo haki na tuna uwezo mkubwa wa kuleta maendeleo,’’ alielezea
WALIMU WA SKULI
Mwalimu mkuu skuli ya Kinyasini
iliyopo Wete Pemba Asha Mbarouk Rashid, amekiri kuwepo kwa kadhia hiyo ya ukosefu
wa mwalimu anaejua lugha za alama kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi wenye
ulemavu.
Hivyo aliomba Wizara ya elimu na mafunzo ya amali, kuwapa kipaumbele
wallimu waliosomea elimu mjumuishi katika ajira jambo ambalo litasaidia
kuondosha tatizo hilo maskulini mwa.
Asha Khamis mzazi wa mtoto mwenye ulemavu wa akili kutoka Micheweni, amesema katika mkoa
wao wa kaskazini Pemba, skuli nyingi hazina
walimu wa kufundisha elimu mjumuishi.
‘’Tunakilio kikubwa sisi wazazi
kwani watoto wetu wenye ulemavu hawasomi, tunawaacha tu majumbani kwa sababu hata
wakienda skuli, hawafahamu chochote kinachofundishwa wanakwenda
wakicheza hakuna walimu wenye taluma,’’
alieleza.
Khatibu Mjaja kutoka Kwale Micheweni alieleza kuwa, yeye mtoto wake
anaulemavu mchanganyiko na ameshindwa kumpeleka skuli, kwani hakuna mwalimu
anaeweza kuzungumza nae na wakaelewana.
‘’Naumia kuona mtoto wangu huyo anakosa haki yake ya elimu kwa sababu
tu ya ulemavu wake, sasa sjui Serikali yetu inampango
gani ya kuimarisha miundombinu ya elimu, ili kuona wanafunzi wenye
ulemavu wanapata elimu,’’anasema.
Mama mzazi wa mwanaunzi mwenye
ulemavu wa viungo kutoka Kijichame Siwawi Omar, alisema kwa kweli walimu wengi wanaofundisha maskulini hawana
taaluma za kufundisha watoto wenye ulemavu.
‘’Ni vyema kuwepo na walimu wenye taluma ya kufundisha wanafunzi wenye
ulemavu, kwani bila ya hivyo siku zote tutawaacha nyuma kimaendeleo,’’ alisema
mzazi
‘njiani tu na ni kuwapa walimu mzigo tu’’ alieleza mzazi.
WANAJAMII
Zahran Mohamed Yussuf mwanajamii kutoka Chake Chake ameeleza kuwa
jamii iliokubwa ya watu wenye ulemavu wamekuwa wakikosa haki yao ya elimu na
wamekuwa wakiachwa majumbani.
‘’Serikali watu wote ni wake na wote wanahitaji haki sawa
hivyo tuikumbushe Serikali yetu ya Zanzibar
kuweka mikakati madhubuti ikiwemo kusomesha kwa wingi walimu
mjumuishi jambo ambalo litapunguza manun’guniko,’’ alishauri.
Sambamba na hilo aliwataka wadau wanaoshughulikia watu wenye ulemavu
kuongeza nguvu ya kuwasemea na kuwatetea
watu hao, ili kuona nawao wanapata fursa mbali mbali za kimaendeleo.
JUMUIA
ZINAZOSHUHULIKIA WATU WENYE ULEMAVU
Kombo Ali Hamad Katibu wa jumuia ya watu wenye ulemavu wilaya ya Wete
mkoa wa kasakazini Pemba, alisema kwa
kweli walimu mjumuishi, maskulini ni
kilio kikubwa kwa
wanafunzi wenye ulemavu.
‘’Wanafunzi wenye ulemavu
wanahaki ya kupata
elimu na kuajiriwa lakini waliowengi
wanakata tamaa hawafikii
ndoto zao kutokana na mazingira magumu yaliopo skulini,’’
alieleza
Amesema kwa sasa elimu
mjumuishi ni jina
tu,
lakini watu wenye ulemavu
hawafaidiki na dhana
hiyo kwani vifaa vya
kufundishia na walimu wenye
taaluma hiyo hawako.
Mudathir Sharif Khamis Naibu Katibu katika Jumuia ya watu wenye
uwalbino kisiwani Pemba, amesema licha ya mchakato mkubwa uliofanyika, ili
kuwepo na elimu mjumuishi lakini bado
wanafunzi wenye ulemavu, wanaendelea kukumbwa na changamoto.
‘’Katika wilaya yetu ya Chake chake kuna wazazi wamekua wakitoka
Ndagoni, Wesha na watoto wao wenye
ulemavu kuwapeleka skuli ya Michakaini, ambapo ndio kituo
kilichochaguliwa kitoe elimu mjumuishi, ni masafa marefu na maisha yenyewe haya tulionayo,’’ alieleza .
Hivyo ni lazima Serikali ikae
itafakari hilo kwani mwisho wa siku kutawafanya wazazi hao kuwakatisha watoto wao na kubaki nao
majumbani mwao kutokana na lengo lao walilokusudia la kupata haki yao ya elimu halifikiwi.
Mratibu wa Jumuia ya watu wasiona
[ZANAB] wilaya ya Chake
chake Suleiman Mansur, ameleza
kuwa elimu mjumuisho bado
haijawanufaisha wanafunzi wenye ulemavu, jambo ambalo linapelekea kufeli kwa
masomo yao.
‘’Kuna baadhi ya walimu
wanapewa taluma ya kufundisha elimu mjumuishi kwa muda wa miezi mitatu kwa
kweli hiyo haitoshi, kama wanataka wenye ulemavu na wao wafaidike na elimu basi ni vyema somo la elimu mjumuishi,’’alieleza.
Mratibu wa ZAPDD Kisiwani Pemba
Khalfan Amour Mohamed, ameeleza kuwa bado waalimu waliowengi hawajakuwa na
taaluma ya kuwafundisha wanafunzi wote wenye ulemavu kulingana na mahaitaji ya
mwanafunzi mwenyewe.
‘’Bado ule ujuzi na uwelewa wa kuwafundisha wanafunzi wenye ulemavu,
mfano wenye ulemavu wa akili, na Viziwi hawajakuwa nao wa kutosha,’’ alieleza
khalfan.
Mwanaharakati kutoka chama cha wandishi wa habari Wanawake Tanzania
Tamwa ofisi ya Pemba Fath-iya Mussa Said amesema suala la walimu wa elimu mjumuishi
bado ni kidogo maskulini watoto wenye
ulemavu wanaendelea kuteseka.
‘’Bado watoto wetu hawajapata walimu wa kuwasomesha mana mwalimu mmoja
ana madarasa manne matano jee atakua na muda gani wa kuwafundisha wenye ulemavu
na wakafahamu bado serikali hili ni tatizo la kuliangalia kwa upeo wa juu
zaid’’ alieleza mwanaharakati.
WIZARA
YA ELIMU
Mratibu wa Elimu
mjumuisho na Stady za maisha ‘EMSM’ Pemba Halima Mohamed Khamis amekiri
kuwepo kwa tatizo hilo la walimu
hususani waalimu wa kuwafundisha viziwi pamoja na wasiona .
‘’Kwa
kipindi cha mwaka jana tulikua tuna idadi ya wanafunzi wenye ulemavu 1710 lakini ukiangalia
walimu wote waliosomea elimu
mjumuishi ni 69 ndani ya Pemba, hivyo bado shida ipo ukiangalia na idadi ya wanafunzi tulionao’’,
alisema Mratib.
Aidha
amesema Serikali kwa kuwajali wanafunzi
wenye ulemavu tayari imeshachukua
idadi ya walimu watakaofundisha elimu mjumuishi kwa ajili ya kuwajiri ili kuondosha tatizo hilo kwa wanafunzi wenye uhitaji maalum.
KATIBA
YA ZANZIBAR
Kifungu cha [10] [g] kinafafanua kwamba Serikali itawekea mazingira
rafiki kwa makundi ya wagonjwa, waliojiajiri, Wazee, Watoto na watu wenye
ulemavu.
Lakini hata kifungu cha 12 [1] kimesema kuwa watu wote ni sawa mbele ya sheria, na
wanayo haki, bila ya ubaguzi wowote kulindwa na kupata haki sawa mbele ya
sheria.
Sheria ya watu wenye ulemavu sheria namba 6 ya mwaka 2022 kifungu cha
28 [1] kimesema kuwa watu wenye ulemavu wanastahiki haki zote za msingi za
binadamu sawa na watu wengine ikijumuisha, haki ya elimu, ikijumuisha mafunzo
ya amali na mafunzo ya kukabiliana na maisha kulingana na aina za ulemavu.
Pia kifungu kidogo cha [2] kimesema kwa kuzingatia masharti ya kifungu
kidogo cha kwanza [1] [a] cha kifungu hiki, Baraza kwa kushirikiana na taasisi
yenye dhamana na masuala ya elimu itahakikisha; watu wenye ulemavu wanapata
elimu na mafunzo ya amali katika ngazi zote na kuwepo na mfumo wa elimu
mjumuishi unaozingatia mahitaji maalum ya watu wenye ulemavu katika ngazi zote
za elimu.
Comments
Post a Comment