WASAIDIZI WA SHERIA PEMBA WAPEWA MBINU JUU YA KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI WA KIJINSIA.



 NA FATMA HAMAD PEMBA.

Wasaidizi wa sheria wamehimizwa kuendelea kutoa elimu kwa jamii ili kuona wanakuwa na uthubutu wa kwenda mahakamani kutoa ushahidi pamoja na kuripoti vituo vya Polisi wakati  kesi zitakapotokezea.

Hayo yamesemwa na Kamanda wa polisi mkoa wa Kusini Pemba Richad Mchovu wakati akifungua kongamano la kutimia kwa miaka 10 yautoaji wa huduma  wa msaada wa kisheria [Lsf]huko Skuli ya Michakaini Chake chake Pemba.

Amesema wasaidizi wa sheria wamekua wakifanya kazi kubwa ya kuibua na kuyaripoti matendo ya udhalilishaji lakini bado jamii inaonekana imegubikwa na tatizo la rushwa muhali.

Hivyo amewataka wasaidizi wa sheria kuongeza jitihada ya kuwailimisha wanajamii madhara ya rushwa muhali pamoja na kuwajengea uwezo wa kusimama mahakamani jambo ambalo lisaidia kuondokana na udhalilishaji wa Wanawake na watoto.

Kamanda huyo ameahidi kutoa mashirikiano ya hali ya juu kwa wasaidizi wa sheria pamoja na ulinzi shirikishi katika mapambano dhidi ya udhalilishaji ili kuona wanawadhibiti wanaofanya makosa hayo na kuona kesi hizo zimepatiwa ufumbuzi.

Akisoma Risala mjumbe wa wasaidi wa sheria katika hafla hiyo amesema bado kuna tatizo la ucheleweshwaji wa uwendeshwaji wa kesi  kuanzia Polisi hadi mahakamani jambo ambalo linawafanya watu wengi kukatamaa ya kufuatilia kesi zao.

Mapema kaimu mratibu wa kituo cha huduma za sheria Zanzibar ofisi ya Pemba Safia Saleh Sultan amesema bado jeshi la polisi linaonekana halijakua tayari katika mapambano dhidi ya udhalilishaji, hivyo basi wakati umefika kuona tasisi zote pamoja na wanaharakati kushirikiana kwa pamoja na kua na kauli ya pamoja ili kuona kila mmoja anatekeleza wajibu wake kwa kuzingatia madili ya kazi yake.

Jumla ya makosa 196 ya udhalilishaji yameripotiwa na kusajiliwa katika vituo vya polisi vya mkoa wa Kusini Pemba kuanzia June mwaka 2020 hadi Julay 2021 ambapo 115 majadala yake yamepelelezwa na kupelekwa kwa DPP, 40 yalifutwa Polisi  kutokana na kukosa ushahidi na kati ya hayo yaliopelekwa kwa dpp  89 yalipelekwa mahakamani.

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.