WANANCHI WATAKIWA KUJITOKEZA KATIKA VIYUO VYA AFYA KUCHOMA CHANJO YA UV19

 

NA FATMA HAMAD FAKI.

Wananchi wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika vituo vya afya kuchoma chanjo ya uviko 19  ili waweze kujikinga na ugonjwa huo.

Wito huo umetolewa na mratibu wa chanjo Kisiwani Pemba Bakar Hamad Bakati wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi katika zoezi la uchanjaji wa chazo hizo, kwa wananchi wa shehia ya Sizini wilaya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Alisema kinga ni bora kuliko tiba, hivyo ni vyema kila mmoja kuhakikisha amechoma chanjo ya uviko 19 jambo ambalo litaepusha kuenea kwa ugongwa huo katika jamii.

Alisema chanjo hiyo itaendelea kutolewa katika kituo cha Afya cha sizini, hivyo wananchi wajitokeze kwa wingi kituoni hapo na kupatiwa chanjo.

‘’Tumeamua kuleta chanjo katika kituo hicho jambo ambalo liwarahisishia wananchi kufuata masafa ya mbali huduma hiyo’’ Alisema mratibu Bakari.

Aidha amefahamisha kuwa wanaostahiki kupata chanjo hiyo ni watu wa zima kuanzia  umri wa miaka  18,wakiwemo na wajawazito.

Baadhi ya wananchi hao wamesema wataendelea kuhamasishana ili kuhakikisha kila mmoja amechoma chanzo hiyo katika kijiji chao.

Huduma hiyo inaendelea kutolewa katika vituo vya afya vilivochagulia ikewemo konde micheweni na wingwi pia inatolewa vijijini kupitia hduma za mkoba.


 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.