WANANCHI WATAKIWA KUIDUMISHANI AMANI
Wananchi wametakiwa kuendelea kuutunza Umoja na mshikamano uliopo sasa ili kuona Amani imetawala na nchi inapinga hatua katika nyanja mbali mbali za kimaendeleo.
Akizungumza
na watendaji wa azaki za kiraia Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Masoud
wakati akifungua kongamono la kumpongeza Rais mwinyi kwa kipindi cha mwaka
mmoja alichokaa madarakani lililofanyika ukumbi wa baraza mji Chake chake
Pemba.
Alisema suala
la kutunza Umoja ni jukumu la kila mtu, hivyo ni vyema kila mmoja kwa nafasi
yake kuendeleza umoja huo ili kuona hakuna vitendo vyovyote viovu
vinavyojitokeza.
‘’Nawasihi
wananchi tuutunzeni umoja wetu na mshikamano wetu ili tuweze kufanya kazi zetu
kwa uhuru’’ alisema Mattar.
Alisema bila
ya kuepo kwa amani si rahisi kupatikana kwa maendeleo, hivyo aliitaka Jamii kujiepusha kufanya vitendo
viovu ambavyo vinaashiria uvunjifu wa amani.
Alisema Rais
Mwinyi kwa kuwajali Wananchi wake ndio
akamua kuunda umoja wa kitaifa ili kuwaunganisha Wazanzibar wote kuwa kitu
kimoja bila ya ubaguzi wowote.
Aidha
alifahamisha kuwa tokea kukaa kwake madarakani Rais Mwinyi kumeanzishwa miradi
mbali mbali ya kimaendeleo nchini ambayo
italeta manufaa kwa Wananchi pamoja na Taifa.
Kwa upande Hidaya
Mjaka Ali kutoka jumuia ya watu wenye
ulemavu, amempongeza Rais Mwinyi kwa kuanzisha mahakama maalumu inayosikiliza
kesi za udhalilishaji jambo ambalo tasaidia
kupatiwa ufumbuzi kwa haraka kesi za
watu hao.
Kongamano
hilo limeandaliwa na mtandao wa asasi za
kiraia [ PACSO] ambapo ujumbe wa kongamano hilo unasema ‘Neema
ya Amani na Umoja wetu, safari ya ujenzi wa Uchumi mpya inaendelea’.
Comments
Post a Comment