UGONJWA WA KOVID 19 BADO NI TATIZO KWA WATU WENYE ULEMAVU
NA FATMA HAMAD FAKI.
Watu wenye
ulemavu wamehimizwa kuendelea kuchukua tahadhari juu ya kujikinga na ugonjwa wa
Uviko 19 katika Jamii zao.
Wito huo
umetolewa na mjumbe wa kamati tendaji wa jumuia ya watu wenye ulemavu [ZAPDD]
Mkubwa Ahmed Omar wakati akifungua mafunzo ya siku moja juu ya kujikinga na
ugonjwa kovid kwa watu wenye ulemavu huko Gombani Chake chake Pemba Alisema
watu wenye ulemavu ni moja ya kundi lililotajwa kuwa hatarini zaid kupata
ugonjwa huo.
Alisema ipo
haja kwa watu hao kuchukua jitihada ya hali ya juu ikiwemo kuosha mikono mara
kwa mara, Kuchoma chanjo pamoja na kuvaa
barakoa wakati wanapokwenda katika mikusanyiko ya watu jambo ambalo litaepusha
kuenea kwa ugonjwa huo.
‘’Nawaomba
jamani tujitahidi sana kuchukua tahadhari kwani ugonjwa bado upoo’’aliwasihi
mjumbe.
Akiwasilisha
mada Afisa kutoka jumuia ya watu wenye ulemavu Zanzibar [ZAPDD] Khalid Abdala
Omar alifahamisha kuwa kwa mujibu wa tafiti ya mwaka 2018 jumla ya watu
wanaoishi na ulemavu wa aina mbali mbali hapa Zanzibar ni 54,335 ambapo ni sawa na asilimia 5.9,
Kati yao,
watu 41,273 sawa na asilimia 7.1 wanaishi Vijijini.
Alisema tafiti hiyo inaonesha kuwa watu wengi wenye
ulemavu wanaishi zaid katika maeneo ya vijijini .
Alisema
licha ya kuwepo kwa watu wengi wenye ulemavu katika maeneo hayo lakini bado
huduma za kiafya hazirishi, hivyo ipo haja kwa tasisi husika kuboresha huduma
hizo ili kuwaondoshea usumbufu wakati wanapofikwa na matatizo.
Aidha
aliwataka Viongozi wa jumuia za watu wenye ulemavu kuwa karibu na jumuia zao
ili waweze kuziibua changamoto zinazowakabili wanachama wao na kuweza kupatiwa
ufumbuzi.
Comments
Post a Comment