HATIMAE MWANAFUNZI WA DARASA LA TANO MWENYE ULEMAVU WA KIUNGO APATIWA MSAADA.


 NA FATMA HAMAD FAKI,PEMBA

Hatimae  Wahisani na wafadhili wameanza kujitokeza kumsaidia  kijana Anifu  Jeilani Isaa mwenye ulemavu wa viungo,  mwanafunzi wa darasa la tano katika skuli ya msingi Ole  ambae ilikua anakabiliwa na changamoto ya baskeli ya maringi mawili kwa ajili ya kwendea skuli.

Akikabidhi msaada huo Katibu wa CCM Jimbo la Ole Yakoub Khalfani Shaha kwa niaba ya Mwakilishi wa Jimbo hilo ambaye pia ni Waziri wa nchi Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Masoud Ali Mohd ,alisema msaada huo umekuja baada ya kuona taarifa zilizo rushwa kwenye mitandao ya kijamii juu ya shida inayo mkabili kijana huyo iliyosababisha kukatisha masomo yake.

‘’Baada ya taarifa zilizo samba mitandaoni juu ya shida zilizokuwa zikimkabili kijana huyo tumeamua kumsaidia ili aondokanae na kero hizo’’ alisema katibu huyo.

Mapema Diwani wa Wadi ya Ole Khadija Henok Maziku  alisema utoaji wa  msaada huo kwa mwakilishi huyo ni katika utekelezaji wa ahadi zake alizoziweka kwa wanajimbo hilo kuhakikisha anatatua kero mbali mbali za wananchi wake.

Akitoa shukrani za dhati Mama mkubwa wa mtoto huyo Fatma Moh’d Omar mara baada ya kupatiwa msaada kwa kijana wake huyo alisema kuwa utaweza kumsaidia kutafuta haki yake ya msingi ya elimu huku akimshauri mwakilishi huyo kuendelea kumsadia.

Aidha bi Khadija aliwataka wazazi wenye watoto walemavu kuacha tabia ya kuwafungia majumbani na badala yake wawapeleke Skuli  pamoja na madrasa ili waweze kujipatia haki yao ya elimu.

Vifaa vilivotolewa na mwakilishi wa jimbo hilo ni pamoja na kibaiskeli,  mabuku, viatu pamoja na Mkoba wa wa Skuli.



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.