UTELEKEZAJI BADO NI TATIZO KWA WANAWAKE NA WATOTO

Utelekezwaji wa wanawake na watoto ni moja ya sababu inayopelekea kuongezeka kwa matendo ya udhalilishaji katika Jamii.

Akizungumza na wandishi wa habari huko ofisini kwake mratibu wa  jumuia ya Tumaini Jipya [TUJIPE] Tatu Abdala Mselem   amesema imebainika kuwa watoto  wengi wanaotelekezwa na wazazi wao hujiingiza katika  masuala ya omba omba na kupelekea kufanyiwa udhalilishaji.

Aidha alifahamisha kuwa akina baba wengi wanapoachana na wenzao wao hawatowi matunzo ipasavyo kwa watoto wao na kupelekea  kukosa  haki  zao  za  msingi.

‘’Wazazi wanapoachana watoto huathirika zaid kwani huwa ni sababu ya wao kutelekezwa na kukosa matunzo’’ alisema Bi tatu.

Kwa upande wake mjumbe wa kamati tendaji kutoka tumaini jipya Ali Yussuf Ali alisema ipo haja kwa viongozi wa dini kuielimisha jamii kuwa na uvumilivu ili  kuepukana na talaka za kiholela jambo ambalo litasaidia kupunguza vitendo hivyo.

Mapema makamo mwenyekiti wa tumaini jipya Suleimana Mohd Iddi alisema licha vitendo hivyo vikionekana kujitokeza kila siku lakini  bado jamii imekua ikiyafumbia macho matendo hayo na kufanya suluhu majumbani  wakidai wanaogopa ugomvi kwenye familia zao.

Jumjla ya majalada 107  ya kesi za udhalilishaji yalipokelewa katika ofisi ya mkurugenzi wa Mashtaka [DPP] kuanzia January hadi Novemba mwaka huu,  majalada 64 yalipelekwa mahakamani, 15 yalirejeshwa kwa upelelezi, 11 yalifungwa, 9 yalimaliza, 5 waliachiwa huru na 3 yaliondolewa.


   

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.