MUHALI BADO NI TATIZO KATIKA KESI ZA UDHALILISHAJI

 


NA FATMA HAMAD PEMBA.

Ushiriki mdogo wa wanajamii dhidi ya utoaji wa ushahidi mahakamani bado  ni changamoto kubwa inayopelekea  kesi za udhalilishaji  kushindwa kupata hatia jambo ambalo linachangia  kuongezeka  kwa vitendo hivyo.

Akizungumza kwa dharura ya mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya mkoani Khatib Juma Mjaja amesema ni muhimu kwa vilabu vya mazoezi kushirikiana na wanaharakati mbali mbali kuielimisha jamii kujua madhara ya rushwa muhali kwani ni adui katika mapambano hayo.

Aidha ameahidi ushikiano sambamba na kuomba umoja huo kuandaa mbinu madhubuti ya kuibua na kuyaripoti matendo hayo ili kuhakikisha wafanyaji wa matukio hayo wanapatikana na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

‘’Sasa ni wakati wa kutekeleza kwa vitendo, hivyo ni jukumu la kila mmoja kusimama kwa nafasi yake kuunga mkono juhudi za kupinga  tatizo hili ambalo limekua ni kilio  kwa wakaazi wa Zazibar’’ alisema mkuu wa wilaya.

Awali akisoma risala mjumbe kutoka umoja wa vilabu vya mazoezi ya viungo  Pemba Shaame Farahani Khamis amesema lengo la bonanza hilo ni kuunga mkono juhudi za Serikali kwani bado changamoto ni nyingi na matendo yanaongezeka hali inayorejeshanyuma vita  dhidi ya udhalilishaji na ukatili wa wanawake na watoto.

Amesema miongoni mwa changamoto hizo nipamoja na rushwa muhali  na kuepo kwa baadhi ya viongozi wasio waadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao.

Nae mkurugenzi wa chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania [ TAMWA- Zanzibar ] Mzuri Issa  Ali ameliomba jeshi la polisi pamoja na mahkama kuunga mkono juhudi hizo kwa vitendo  kwani kesi nyingi zinafeli hazipatiwi hukumu kwa kisingizio cha kukosekana kwa ushahidi.



Bonanza la umoja wa vilabu vya maazoezi ya viongo pemba ni miongoni mwa maadhimisho ya kilele cha siku 16 za kupinga udhalilishaji sambamba na uzinduzi wa umoja huo ambapo jumla ya vilabu 17 vimeshiriki kutoka sehemu tofauti kisiwani Pemba.

 

 


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.