WAZAZI WAOMBWA KULEA WATOTO WAO KATIKA MALEZI YA PAMOJA


Wazazi  wametakiwa kurejesha malezi ya pamoja katika kuwalea watoto wao jambo ambalo litasaidia kupatikana kwa kizazi chenye madili bora.

 Hayo yamesemwa na kaimu mratibu wa kituo cha huduma za sheria  Safia Saleh Sultan wakati akizungumza na wanakikundi cha chapa kazi cha wanakisomo kilichopo  Kwale Gombani Chake chake Pemba.

Alisema kukosekana kwa kizazi chenye madili ni moja ya sababu inayopelekea kuongezeka kwa vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia, hivyo wakati umefika kwa wazazi kushirikiana kwa pamoja ili kupunguza tatizo hilo hapa nchini.



 Akiwasilisha mada katika mkutano huo Khadija kutoka kituo cha huduma za sheria  amewataka wazazi  fuatilia nyenendo za  watoto wao wakati wanapokwenda skuli na madrasa ili kuwalinda na vitendo viovu vikiwemo vya udhalilishaji.

Samba mba na hilo amesema endapo jamii itatoa huduma stahiki kwa family zao inaweza ikasaidia watoto kujiepusha kujitumbwikiza katika vigenge viovu ambavyo vinachangia kwa kiasi kikubwa wimbi la udhalilishaji.

Nao wanakikundi hao wameiomba Serikali kuzipitia upya sheria ili kuona  adhabu zinatolewa kwa jinsia zote mbili wakati itakapobainika kuwa na makubaliano ya hiyari kwa pande mbili husika [MKE NA MUME].



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.