ATIWA MBARONI AKIDAIWA KUMLAWITI MLEMAVU WA AKILI
Msifunzwa ni mamae hufunzwa ni ulimwengu hii imekuja baada ya Nuhu Kombo Nuhu mwenye mumri wa miaka 22 akihemea polisi kwa tuhuma za kumlawiti kijana wa 18 mwenye ulemavu wa akili na mdomo.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi mama mzazi wa kijana huyo amesema ailikua yupo nae
nyumbani badae akatoka na hakurudi
tena na alianza kumtafuta ila hakumuona.
Alisema kuwa
baada ya muda mrefu kupita
aliletewa nyumbani na msamaria mwema na kumuambia huyu mtoto wako
nimemkuta Vichakani akiwa anafanyiwa udhalilishaji
na Nuhu Kombo Nuhu.
Alifahamisha
kuwa baada ya hapo aliendelea kumuhoji na kumuambia
kuwa hii ni kawaida yake kumchukua na kumpeleka vichakani kumfanyia kitendo hicho
‘’Nilipo
muhoji aliniambia ashazoea kunifanyia hivi
na ananiambia atanipa pesa na simu ya tachi’’ alieleza mama mzazi.
Aidha mama
huyo alisema kuwa baadhi ya wanafamili wa mtuhumiwa huyo wamekua wakimtolea maneno mabaya huku wakimtaka wafanye suluhu ili kesi isiendelee.
‘’Kitendo
hicho cha kinyama alichofanyiwa mwanangu nimekipokea kwa masikitiko makubwa
kutokana na hali ya mwanangu kwani hana
akili na hasemi, hivyo siko tayari na suluhu nitasimama kidete mpaka haki
itendeke’’ alieleza mama mazazi.
Hivyo
aliviomba vyombo vinavyohusika kutoa adhabu kali kwa muhalifu huyo ili iwe dawa
kwa wengine.
Sheha wa
shehia ya Sizini Nassor Kombo Khator alisema kitendo hicho cha kinyama
kimemuhuzunisha hivyo amewaomba wazazi na walezi kuwa karibu zaid na watoto
kwani udhalilishaji umeenea kila sehemu.
Aidha
aliwashauri wanajamii kuondosha muhali na kuwa na ujasiri wa kuyafichua na
kuyaripoti matendo haya katika vyombo vya sheria jambo ambalo litapunguza masuala haya.
Sambamba na
hilo kamanda alisema vitendo vya udhalilisha vimeshamiri hivyo wakati umefika kwa wazazi kuka na
watoto wao na kuwaelimisha juu ya madhara ya udhalilishaji jambo ambalo
litawafanya kuwa na woga juu ya masuala hayo.
Amesema kila
mmoja ni mlemavu mtarajiwa hivyo ni wajibu wa kila mmoja kuwalinda watu hao ili
kuwaepusha na udhalilishaji .
Hivyo
amesema watahakikisha wanaifuatilia kesi
hiyo mpaka haki ya kijana huyo ipatikane.
Comments
Post a Comment