MELI KUBWA LA WATALII KUTOKA UFARANSA LATUA KISIWANI PEMBA.
NA FATMA
HAMAD PEMBA.
JUMLA ya
watalii 69 wamewasili kisiwani Pemba kwa meli maalumu, kwa lengo la kujionea
vivutio mbali mbali vya utalii vilivyomo Kisiwani humo.
Watalii hao raia wa Ufaransa wamewasili Kisiwani Pemba kwa ziara
ya siku Moja, kwa kutumia Usafiri wa meli aina ya LE BELLOT, wameweza
kutembelea na kujionea vivutio vya utalii.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwapokea
watalii hao, kwa Niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mkoa wa Kusini Pemba, Mkuu wa Wilaya
ya Mkoani Khatib Juma Mjaja, alisema ujio wa watalii hao ni kukitangaza kisiwa
cha Pemba kiutalii kupitia vivutio mbali mbali vilivyomo.
Alisema ujio wao utaweza kuwanufaisha wafanya biashara na
wajasiriamali, kuuza na kutangaza bidhaa na biashara zao kimataifa.
“Kwa sasa ni wazi kuwa Kisiwa cha Pemba kimeanza kufunguka
kiutalii, ujio wao utaweza kuonyesha dunia kuwa Pemba kuna vivutio vingi vya
Kiutalii, Pemba ni sehemu salama ya watalii kutembea”alisema.
Aidha Mkuu huyo alisema ni meli ya pili hiyo kuwasili katika
kisiwa hicho, kwani 2018 meli kama hiyo iliwasilia huku wakiitikia wito wa Rais
wa Zanzibar kutaka kuongeza idadi ya watalii kutoka 35,000 hadi laki 150,000
ifikapo 2025.
Hata hivyo aliwataka wajasiriamali Kisiwani Pemba, kujiandaa
kuitalii kupitia shuhuli mbali mbali ikiwemo Kilimo, Ufugaji na Uvuvi.
Afisa Mdhamini Wizara ya Utalii na Mambo ya kale Pemba Zuhura
Mgeni Juma, alisema mikakati ya Wizara yake ni kuhakikisha wanavitangaza
vivutio vya utalii vilivyopo ndani ya Kisiwa cha Pemba pamoja na kuibua vivutio
vipya.
Naye Mkurugenzi wa Shirika la Bandari Tawi la Pemba Abdulla
Salim Abdulla, amesema sababu ya meli hiyo iliyokuja na wageni hao kushindwa
kufunga gati bandarini hapo ni kutokana na ukubwa wa meli hiyo kuwa na Mita 130
wakati bandari inamita 11`5.
Alisema kwa sasa serikali ipo katika mpango wa utanuzi wa
bandari hiyo, kwa lengo la kuweza kufunga gati meli mbali mbali kubwa na za
kimataifa, ikiwemo meli za makontena na kuweza kushusha mizigo ndani ya bandari
hiyo.
“Hii ni meli ya kwanza kwa Afrika kwa mwaka huu kuja na watalii,
hii inadhihirisha kuwa bandari ya Pemba ni salama kwa meli na abiria wake kuja,
hili litaweza kuitanganza Pemba kidunia kuwa sehemu salama kutembea”alisema.
Mdhamini wa kamisheni ya Utalii Pemba Hamadi Amini Ali, alisema
kufika kwa wageni hao ni moja ya kuitangaza kidunia kuwa ni sehemu salama kwa
wageni, pia kuwa na vivutio adimu wakiwemo popo wa pemba ambao hawapatikani
duniani kokote.
Naye afisa Utumishi wa Wizara hiyo Fatma Salim Ali, alifahamisha
kuw aujio wao kutaweza kuongeza mapato kwa serikali na wafanyabiashara, kwani
watalii hao watalipa katika taasisi zinazohusika, kununua biashara kwa
wajasiariamali.
Mkurugenzi wa kampuni ya East African Holiday iliyowaleta
watalii hapo Pemba Duwe Lazaro Daudi, alisema watalii hao watarudi tena Pemba Disemba
29, kwa kutembelea tena maeneo mbali mbali.
Aidha alishukuru serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar [SMZ] na
yajamuhuri ya Mungano wa Tanzania [SMT] katika kusaidia kampuni hiyo
inafanikiwa kuwaleta wageni hao, ndani ya Visiwa vya Zanzibar na baadae kuelekea
Kilwa.
Fatma Khamis Haji mfanyabishara wa Embe katika soko la Matunda
Chake Chake, alisema ujio wao utaweza kutanua bishara zao, pamoja na kupata
fedha za kigeni.
Naye Mohamed Salehe Ali Muuza haluwa maarufu soko la Jua kali
Chake Chake, aliipongeza Serikali ya Mungano [SMT] kwa kutangaza Kisiwa cha
Pemba kiutalii, pamoja na watalii hao kujuwa ladha ya halua ya Pemba ambayo
itakuwa ni kivutio kwa watalii wengine.
Hata hivyo ziara ya watalii hao ndani ya ksiiwa cha Pemba,
imezingatia taratibu zote za afya, ikiwemo uvaaji wa barakoa, unawaji mikono
kwa kutumia vitakasa maalumu.
Comments
Post a Comment