WAZAZI WATAKIWA KUTOA MATUNZO STAHIKI KWA FAMILIA ZAO


Wazazi na walezi wamehimzwa kuendelea kutoa huduma stahiki kwa watoto wao jambo ambalo litaepusha kufanyiwa kwa  udhalilishaji wa kijinsia  kwa watoto.

Ushauri huo umetolewa na Siti Habibu Mohd kutoka kituo cha huduma za Sheria ofisi ya Pemba wakati akitoa elimu juu ya kuripoti matendo ya udhalilishaji  kwa wanafunzi wa Skuli ya Madungu Msingi alisema bado suala la udhalilishaji linaendelea kufanyika kila siku , hivyo ni vyema wazazi kuwa na ukaribu wa hali ya juu pamoja na kuwapatia huduma  ili kuwalinda na vitendo hivyo.

‘’Nawasihi wazazi wenzangu tujitahidi kuwahudumia watoto wetu ili tuwalinde na vitendo viovu’’ alisema Bi siti.

Sambamba na hilo aliwataka wanajamii kushirikiana na vyombo vya kisheria kwa kuwafichua watendaji wa makosa hayo pamoja na kutoa ushahidi mahakamani jambo ambalo litapunguza matendo hayo.

Aidha aliwataka wanafunzi hao kutoa tarifa kwa watu wao wa karibu  ikiwa ni pamoja na wazazi, walimu wao, wakati wanapofanyiwa vitendo vya udhalilishaji  ili kujinusuru na janga hilo.

‘’Udhalilishaji unafanyika kila eneo hivyo tumeamua kuwapa elimu wanafunzi hawa ili wawe na uthubu wa kuyaripoti.

Alisema bado kuna watoto wamekuwa wakifanyiwa vitendo hivyo lakini  hawana uthubutu wa kuyaripoti katika sehemu husika na kupelea kuendela  siku hadi siku.

Alisema lengo la kutoa elimu hiyo kwa wanafunzi hao ni shamra shamra maadhimisho ya siku 16 ya kupinga udhalilishaji wa kijinsia.



 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.