JAMII YAHIMIZWA KUWATUNZA NA KUWATHAMINI WATU WENYE ULEMAVU.
kikundi Cha Mazoezi ya viungo cha Gombani Fitnes Senter kilichopo chake chake kimemtembelea na kumfariji kijana Asaa Khamis mwenye ulemavu wa Viungo Mkaazi wa Shumba ya Vyamboni wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba kufuatia habari iliyorushwa katika Blog ya Pemba ya leo iliyo muhusu kijana huyo akihitaji msaada wa kupatiwa mtaji kwa ajili ya kuendeleza biashara zake.
Akizungumza mara
bada ya kumfariji kijana huyo katibu wa
Kikundi hicho Khalfan Amour
Mohd alisema mbali ya kukindi hicho kufanya mazoezi pia kimekua kikifanya harakati mbali mbali za
kijamii kama vile kusaidia watu wenye ulemavu, pamoja na kupiga vita masuala ya
udhalilishaji hususan kwa walemavu .
‘’Unajua sisi
tumeguswa na makala iliyorushwa kwenye mtandao inayomzungumzia Kijana Asaa
jinsi anavyopata shida kutokana na ulemavu wake tukaona ipo haja kumfariji kwa
vile na sisi ni walemavu watarajiwa’’alisema Khalfani.
Alisema watu wenye
ulemavu wanakumbana na changamoto nyingi katika maisha yao hivyo ipo haja
kuangaliwa, na kushirikishwa katika fursa mbali mbali za kimaendeleo.
Hata hivyo katibu
huyo aliviomba vikundi vyengine vya mazoezi kuiga mfano huo wa kusadia makundi
maalumu na hata harakati nyengine za kijamii.
Comments
Post a Comment