UMOJA WA VILABU UNAWATAKA WANANCHI KUJITOKEZA KATIKA MADHIMISHO YA SIKU 16 YA KUPINGA UDHALILISHAJI

 Katika kuelekea maadhimisho ya   siku  16  ya  kupinga udhalilishaji wa kijinsia Zanzubar Umoja wa vilabu vya mazoezi   kisiwani Pemba umedhamiria kufanya bonanza malum la kuadhimisha siku hiyo jumamosi ya  tarehe 11 mwezi  huu huko katika Uwanja wa michezo Gombani Chake chake.

Akizungumza na wandishi wa habari katika ofisi za Tamwa Mkanjuni Chake chake katibu wa jumuia ya umoja wa vilabu vya mazoezi kisiwani Pemba Khalfan Amour Mohd alisema  umoja huo umeamua kuadhimisha siku hiyo ili kuunga mkono juhudi za Serikali katika mapambano dhidi ya ukatili wa wanawake na watoto ambao umekua ukiwakumba mara kwa mara katika jamii.

Alisema kumekuwepo na vitendo vingi vya ukatili wa kijinsia ambavyo huakumba zaid Wanawake na watoto, hivyo wameona ipo haja nawao kuchukua jitihada za makusudi  za kuzipigia kelele zile kero ambazo zinawakumba wanawake na watoto katika jamii na kuzifikisha katika mamlaka husika ili kuona haki inatendeka.

‘’Tumeona kwa vitendo vya udhalilishaji vinafanyika katika jamii zetu tunazoishi, hivyo tumeamua na sisi tujitolee na tuweze kushirikiana na wadau mbali mbali kupiga vita vitendo hivy’’ alisema katibu.

Alisema  ili kupunguza tatizo hili hapa Nchini ni vyema kila mmoja kwa nafasi yake kuchukua hatua ipasavyo pamoja na kufanya kazi zao kwa uadilifu kwa misingi ya sheria na nidhamu.


Kwa upande wake mkurugenzi wa chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania [ Tamwa] Mzuri Issa  amesema kufuatia juhudi zinazochukuliwa na wanaharakati mbali mbali kuielimisha jamii juu ya madhara yatokanayo  udhalilisha wananchi wamehamasika katika kuziripoti kesi za udhalilishaji kwa mamlaka husika ukilinganisha na miaka iliyopita.

Aidha ameipongeza Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kwa  kuweka mikakati mbali mbali ili kuona kesi hizi zinaendeshwa kwa haraka na kupatiwa hukumu.

Bonanza hilo linatarajiwa kufanyika  Disemba 11 mwaka huu,ambalo limeandaliwa na umoja wa vilabu vya mazoezi kwa kushirikiana na Chama cha wandishi wa habari Wanawake Tanzani [TAMWA], Jumuia ya watu wenye ulemavu kisiwani pemba [ZAPDD]  bonanza hilo ambalo litakua na matembezi kuanzia madungu chake chake hadi uwanja wa Gombani.



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.