JAJI MKUU ZANZIBAR ATAKA WANAFUNZI WA VYUO VYA MAFUNZO KUPATIWA ELIMU YA USHAURI NASAHA

 

                               NA FATMA HAMAD, PEMBA

Mahikimu wa mahakama za kadhi, Makamanda wa Vyuo vya mafunzo kisiwani Pemba wametakiwa kushirikia na Idara ya Msaada wa kisheria  kuwapa  elimu  ya  ushauri  nasaha wanafunzi   wa  Vyuo  vya  mafunzo ili waweze kubadilika na kuwa na tabia njema.

Agizo hilo limetolewa na  Jaji mkuu wa Zanzibar Ramadhan Khamis Abdala wakati akizungumza na wanafunzi pamoja na Makamanda wa Vyuo vya mafunzo kisiwani Pemba.

Alisema wengi wanaofikwa na mtihani wa kwenda kwenye  vyuo vya mafunzo wanahisi kama wameonewa, hivyo ni vyema kuanzishwa utaratibu wa kupewa ushauri nasaha ili waweze kuondokana na mawazo hayo,na kuona watakaporudi katika familia zao  wamebadilika tabia na kuwa Raia wema.

‘’Wenzetu hawa  wanapokuja humu vyuoni huwa wanathirika kisaikologia, na kuhisi Serikali imewaonea hivyo ni budi kuwapa Mawaidha pamoja na ushauri nasaha ili ziweze kurudi  akili zao, alisema.

Aidha alisema ni vyema kupatiwa misada midogo midogo ikiwemo Tende, hususan katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadani, kwani kutawafanya wafunge Ramadhani katika hali ya amani na utulivu licha ya kuwa hawako katika mikono ya familia zao.

 

Kwa upande wao wanafunzi wa vyuo vya mafunzo walisema changamoto kubwa inayowakwaza ni ucheleweshwaji wa kupata Prosija za kesi zao wakati wanapomba kwa ajili ya kukata rufa.

‘‘ kukata rufaa ni haki yetu hivyo mtu akiomba prosija apewe kwa haraka tunawaomba,walisema.

Aidha kwa upande mwengine  waliitaka Serikali ya Mpinduzi Zanzibar kuongeza mahakimu wa Mahakama ya Rufaa kisiwani Pemba kwani kufanya hivyo kutapunguza wimbi kubwa la ucheleweshaji wa uwendeshaji wa kesi katika Mahakama hiyo.

‘’Kesi za Mahakama za Rufaa zinachelewa sana kwani kuwepo na mtendaji mmoja ni shida, tunaomba waengezwe tunakaa sana gerezani tunaumia,walieleza.

 Nao viongozi wa vyio vya mafunzo walisema kitendo  hicho kilichofanywa na Jaji  mkuu na Timu  yake  kutembelea Vyuo vya mafunzo ni kitendo cha kupigwa mfano, kwani kutasaidia kutatuliwa kwa baadhi ya  matatizo yanayowakumbwa wanafunzi vyuoni  hapo.

Ziara hiyo ya kutembelea vyuo vya mafunzo ni utaratibu wa viongozi wa Mahakama  kila ikikaribia siku ya sheria kuvitembelea vyuo vya mafunzo na kusikilizi kero za wanafunzi.

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.