WANDISHI WA HABARI PEMBA WAPIGWA MSASA

 


                    NA FATMA HAMAD

Wandishi wa habari wametakiwa  kuielimisha jamii kufahamu     masuala ya Afya ya uzazi, ili kufahamu afya zao, na kuweza  kupata tiba  sahihi, jambo ambalo litasaidia kupunguza  vifo vya mama na mtoto.

Ushauri huo umetolewa na afisa mradi wa afya ya uzazi, wakati akielezea kuhusu mradi huo wa uzazi salama  Zaina Abdala Mzee kwenye  mafunzo ya siku tatu ya kuwajengea uwezo wandishi wa habari, kuandika habari zinazo husu masuala ya afya ya uzazi,  yaliofanyika katika ukumbi wa Tamwa Chake Chake Pemba.

Alisema kwa mujibu wa tafiti kutoka wizara ya afya,  vifo vya mama na mtoto  bado ni changamoto inayoikumba Jamii.

Alisema wandishi wa habari wana nafasi kubwa katika jamii, hivyo ni vyema kuwandika habari pamoja na makala ambazo zitaisaidia jamii kufahamu masuala ya  afya ya uzazi ili waweze kufika vituo vya afya kufanyiwa uchunguzi na kupatiwa matibabu.

‘’Nyinyi waandishi wa habari mnaaminika zaidi katika jamii, hivyo ni vyema mkayatumia mafunzo haya kwa kuielimisha jamii ili kuona lile lengo hasa la mradi huu la kupunguza tatizo la vifo vya mama na mtoto limefikiwa’’, alieleza afisa mradi.

Alifahamisha kuwa wameamua kuleta mpango huo ili wandishi wa habai waweze kuielimisha jamii, ili kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Alisema suala la afya ya uzazi si suala la mwanamke peke yake bali linahitajika kwa kila mtu jambo ambalo litasaidia jamii kuondokana na maradhi.


Mapema  akifungua mafunzo hayo afisa Ufuatiliaji na  tathmini kutoka Chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania [Tamwa]  Mohamed  Khatib  Mohamed  alisema  lengo la kuwapatia mafunzo hayo ni kuwasaidia wandishi wa habari  kuibua changamoto zinazo wakumba wanajamii, katika upatikanaji wa huduma ili ziweze kusikika na kupatiwa ufumbuzi.

Akiwasilisha mada juu ya mazingira ya kidini na kitamaduni kuhusu haki ya afya uzazi, Sheikh  Abdalla Nassor Abdalla  kutoka jumuia ya maimamu Zanzibar ofisi ya Pemba [ JUMAZA] alisema ni vyema kwa vijana watakaoingia kwenye ndoa kupima afya zao kabla ya kuingia kwenye ndoa.

Alifahamisha kuwa  afya ya uzazi inanzia pale kipindi cha ujauzito hadi kufikia kwenye makuzi, malezi, na matunzo  ya mtoto.

Mradi huu wa afya ya uzazi ni mashirikiano ya Tamwa Bara na Tamwa Zanzibar chini ya ufadhili wa wellsring Phianthrepi und[WP] kutoka nchini Marekani.

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.