ALIEMNAJISI MTOTO MWENYE ULEMAVU WA AKILI AENDELEA KUSOTA RUMANDE

 

                         Na Fatma Hamad Pemba.

Mahakama  ya mkoa A wete imeighairisha kesi ya kunajisi mtoto mwenye ulemavu wa akili inayomkabili kijana Khamis Salim Ali  mwenye umri wa miaka 27 mkaazi wa Selemu  wilaya ya wete mkoa wa Kaskazini Pemba.

Imedaiwa  mahakamani  hapo  siku ya  tarehe  5/2/2023  majira ya  skumi  za  jioni huko Selemu Wete ulimuingialia mtoto wa Kiume   mwenye  umri  wa  miaka  12 ambae ni mwenye ulemavu wa akili  jambo ambalo ni kosa kisheria.

Mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka DPP Juma Mussa Omar amesema kuwa kesi hiyo ilikua katika hatua ya utetezi lakini hatutoendelea kwani hakimu anaesikiliza kesi hiyo  hayupo.

Hakimu wa mahakama ya mkoa A Said Hemed  amesema   hakimu anaendesha kesi za udhalilishaji hayupo mahakamani amepata dharura ya kikazi nje ya Pemba kesi hiyo itarudi tena mahakamani hapo  tarehe 12/7/ 2023 na kuendelea na utetezi.

‘’Naighairisha kesi hiyo hadi tarehe 12/ 7/ 2023 na mtuhumiwa ataendelea kukaa rumande’’ alieleza hakimu Said.

Kunajisi mtoto mwenye ulemavu wa akili  imedaiwa ni kosa kinyume na kifungu cha [116] [1] cha sheria nambari 6/2018 sheria ya  Zanzibar.

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.