JAMII YAPEWA ONYO

 


                               NA FATMA HAMAD PEMBA

Jamii imehimizwa kuendelea kuziripoti katika vyombo vya sharia  kesi za udhalilishaji, na sio  kuzikalia kitako na kuzifanyia suluhu kifemilia.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Hakimu wa mahakama maalum ya kupambana na udhalilishaji iliyopo Wete mkoa wa Kaskazini Pemba, Ali  Abdul Rahman Ali amesema Serilaki imefanya jitihada mbali mbali ikiwemo kuanzisha mahakama maalum ili kuondosha tatizo hilo Nchini.

Alisema licha ya elimu inayoendelea kutolewa kila siku kwa wanajamii,  ili kufahamu madhara ya udhalilishaji, lakini bado jamii imegubikwa na wimbi la rushwa muhali  na  badalayake kuzifumbia macho na kuzifanyia suluhu wenyewe kwa wenyewe, hali ambayo inapelekea kuongezeka kwa udhalilishaji.

‘’Ndugu wanajamii, tusipokuwa makini na tukiendelea kumuonea huruma mdhalilishaji, bado tutaendelea kuutilia mbolea udhalilishajikatika jamii zetu,’’ alieleza hakimu.

Hakimu huyo aliendelea kufahamisha kuwa zipo baadhi ya familia huziripoti kesi zao, lakini mwisho wa siku hawajitokezi mahakamani na kutoa ushahidi, na badala yake kubakia kuitupia lawama mahakama.

‘’Mtaendelea kutulaumu kila siku mahakimu tunakula rushwa, tunapewa hongo, lakini bila ya kuepo na ushahidi hatuwezi kumtia mtu hatiani,’aliesema hakimu Ali.

Akitoa ushuhuda mmoja wa wahanga wa tukio la udhalilishaji kutoka wilaya ya Micheweni, alisema baada ya mtoto wake kudhalilishwa na kuenda kwenye vyombo vya sharia, baadhi wanafamilia walimtenga na kumuekea vikao ili  waimalize kimya kimya, kwani  mfanyaji alikua ni ndugu wa familia , hivyo atasababisha ugonvi.

‘’ Sikujali maneno ya watu, wala  sikukubali kuimalizia mtaani, niliendelea kuifuatilia  kesi yangu na mwisho wa siku  mtuhumiwa  kafungwa jela miaka 7,’’ alisema muhanga wa udhalilishaji

Nao baadhi ya wananchi kutoka mkoa wa kaskazini Pemba walivitaka vyombo vinavyotoa haki,  kufanya kazi zao kwa uwadilifu ili kuona kila mmoja anapata haki yake, na sio kuwangalia wenye vipato vya juu tu.

‘’Mahakama maalum imewekwa iwe mkombozi kwa watu wote, hivyo tunawaomba mnaosimamia hizi kesi kutenda haki, ili wanyonge nawao tupate haki zetu pindi tunapofikwa na kadhya za udhalilisha,’’ walisema wananchi.

Jumla ya kesi 134 za udhalilishaji zimeripotiwa katika mahakama maalum ya kupambana na udhalilishaji mkoa wa Kaskazini Pemba, kuanzia mwaka 2021 hadi June 2023, ambapo 2021 kuliripotiwa kesi 55, 2022 63, na January hadi June 20233 kesi 15.

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.