JESHI LA KUJENGA UCHUMI [JKU] LAPEWA NENO

                                 NA SAID ABRAHMAN PEMBA.

NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt, Abdalla Juma Sadalla (Mabodi) amelitaka jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar (JKU) kujitoa na kutoa elimu Kwa wananchi juu ya kilimo Bora ambacho kitaweza kuwaletea tija.

Alisema kuwa ni vyema Kwa wataalamu wa kilimo wa jeshi hilo kutoa elimu zaidi Kwa wakulima ili tija iweze kupatikana.

 Mabodi aliyesema hayo huko katika Viwanja vya maonesho ya siku chakula Duniani yanaendelea huko  Chamanangwe Wilaya ya Wete wakati akizungumza na waandishi wa habari.

 Alieleza kuwa Jku ni jeshi la Kujenga Uchumi hasa kwani limekuwa likifanya vizuri katika sekta ya uzalishaji mali.

 "Nina Imani kubwa kuwa huko mbele ya safari Kuna hatari ya katika dhana ya Uchumi wa bluu kukawa naushindani Mkubwa baina ya Jku na KM KM Kwa kiasi Fulani," alieleza Mabodi.

 Sambamba na hayo Mabodi alifahamisha dhana nzima ya kuanzishwa Kwa Jku ni kutoa taaluma mbali mbali Kwa Vijana wa kizanzibari ili waweze kujitegemea katika maisha yao na kuacha kutegemea ajira kutoka Serikalini.

 "Nilipongeze Jku Kwa jitihada zake za kuweza kuwafundisha vijana wetu mbali mbali za stadi za maisha,ukakamavu,uzakendo was nchi Yao,kwani asilimia kubwa ya Wananchi wetu ni vijana," alisema Mabodi.

 "Serikalini tuna ajira ndogo na hivyo ni vigumu kusema kuwa wananchi wote waajiriwe, ninafahamu hivi Sasa Kuna vijana wengi wanafunzwa ujasiriamali kupitia Jku,wengine wanajifunza ufundi wa aina mbali mbali na wengine wanajinza mambo ya utalii na ulinzi," alisema Mabodi.

 Mapema naibu huyo aliipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Kwa kutekeleza vyema ilani ya Chama Cha Mapinduzi Kwa vitendo.

 Maonesho ya siku ya Chakula Duniani huadhimishwa kila ifikapo Octoba 10 ya kila mwaka ambapo wananchi kutoka sehemu mbali mbali za Kisiwa Cha Pemba hupata fursa ya kutembelea maeneo ya maonesho hayo yaliyopo Chamanangwe Wilaya ya Wete, Ujumbe wa mwaka huu "Haachwi mtu nyuma,uzalishaji Bora,lishe Bora, mazingira Bora na maisha Bora Kwa wote".

 

 


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.