WANDISHI WA HABARI WAPEWA MBINU.

 


FATMA HAMAD PEMBA.

Wandishi wa habari  Nchini wamekumbushwa  kuitumia mitandao ya kijamii kwa kuandika habari zenye ukweli na  zenye  ubora  ili kuepuka    kuingia  katika migoghoro isio  ya lazima.

Ukumbusho huo umetolewa na Mwenyekiti wa Jumuia ya wandishi wa habari Pemba Pres Clab [PPC]  Bakar Mussa Juma wakati akizungumza na wandishi wa habari wa mitandao katika mafunzo  juu ya ulinzi na usalama wa mitandao ya kijamii huko ofisi ya  Ppc  Chake chake Pemba.

Amesema mitandao ya kijamii ndio chombo kinachofikisha ujumbe haraka kwa jamii hivyo ni vyema kuwa makini wakati wanaporusha habari zao ili iweze kuwajenga na kuwa huru katika kazi zenu.

Amesema vyombo vya habari ndio sauti ya wasio na sauti  hivyo sasa ni wakati wa  Wandishi kubadilika  na  waweze kuandika habari zenye uhakika ambazo zitaleta tija kwa Jamii.

 ‘’Mitandao ya kijamii  ndio chombo kinachofikisha ujumbe kwa haraka katika jamii hivyo lazima muwe makini sana katika kutumia hii mitandao  kwani kumekua na watu wakidukua habarinzenu mnazoziweka  kwe mitandao’’ alisema katibu.

Aidha katibu huyo amewahamasisha  wandishi  ambao bado hawajajiunga na Clabu ya wandishi wa  habari  ili waweze kupata fursa mbali mbali za kimaendeleo ambazo zimekua zikijitokeza clabuni hapo.

Mwenyekiti wa PPC Bakar Mussa Juma akizungumza na wandishi.


Mapema mratibu wa Pemba Press Clab [PPC] Mgeni Kombo Khamis  amewataka wandishi waliopata mafunzo hayo kuyachukua na kuyafanyia kazi ili waweze kuandika vyema habari zao.

Akitoa mafunzo  mkufunzi wa mafunzo hayo  Haji Nassor Mohad  amewasisitiza  wandishi  hao  kuifikisha  taaluma  hiyo kwa wandishi wenzao  ili  nawao wapate kunufaika na elimu hiyo.


Nao wandishi waliopata mafunzo hayo wameahidi kuyatumia vyema wakati wanapoandika habari zao jambo ambalo litasaidia kundika habari zisizo na migogoro.

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.