WAZAZI WAPEWA MBINU YA KUWALEA WATOTO WENYE ULEMAVU WA AKILI.

 

                       NA FATMA HAMAD PEMBA 12/10/2022.

Wazazi na walezi wanaoishi na watoto wenye ulemavu  wa akili wametakiwa kuzidisha ulinzi zaidi kwa watoto hao ili kuwalinda na vitendo vya udhalilishaji.

Wito huo umetolewa na mratibu wa jumuiya ya watu wenye ulemavu kisiwani Pemba [ZAPDD]  Khalfan Amour Mohd wakati akizungumza na wanachama wa jumuia ya watu wenye ulemavu wa akili huko Kiuyu mbuyuni wilaya ya Micheweni mkoa wa Kasakazini Pemba kufuatia kuzuka kwa vitendo vya udhalilishaji wanavyofanyiwa watu wenye ulemavu wa akili.

Alisema  wapo watu  wamekua wakiwachukua watoto wenye ulemavu wa akili kwa ajili ya  kumaliza haja zao za matamanio, hivyo wazazi mnajukumu kubwa la kuhakikisha mnakuwa na ulinzi wa hali juu ili kuhakikisha mda wote wapo katika hali ya amani na usalama vijana hao.

‘’Licha ya halingumu mlizonazo  za kimaisha  lakini tuwashuhulikieni watoto wetu wenye ulemavu tusiwabeze jamani’’ alisema mratib khalfan.

Kwa upande wake  msaidizi mwenyekiti wa jumuia ya watu wenye ulemavu wa akili [ZAPDD] mkoa wa Kaskazi Pemba Zubeir Iddi Khamis  aliwataka wanajumuia hao kuvifichua vitendo  viovu wanavyofanyiwa  watoto wenye ulemavu ikiwemo udhalilishaji ili  kufikishwa katika vyombo vya kisheria.

Nae Mjumbe kutoka Shijuwaza Aziza Alawi Mussa aliwashauri wazazi wanaoishi na watoto wenye ulemavu kuziibua kero na changamoto zinazowakumba watoto hao kama vile vibaskeli vya kutembelea ili ziweze kupatiwa ufumbuzi.

‘’Tusiwadharau watoto wetu wenye ulemavu huu ni mtihani mungu ametujalia ikiwa anashida ya Kigari, Miwani toeni raarifa tunao wenzetu wa inclusive watatusaidia jamani’’ alifahamisha bi Aziza.

Kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu cha 15 kifungu kidogo cha kwanza kinasema kila mtu anastahili kuheshimiwa na kupata hifadhi kwa nafsi yake, maisha yake binafsi na Nyumbani kwake, na pia heshima na hifadhi ya maskani yake na mawasiliano yake.

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.