HIZI HAPA CHANGAMOTO WANAZOZIPATA WATU WENYE ULEMAVU.



                          NA FATMA HAMAD PEMBA. 9/10/2022

Licha ya  juhudi  zinazochukuliwa na Serikali pamoja na mashirika mbali mbali yanayoshughulikia  watu wenyeulemavu  ili kuona watu wenye ulemavu wanaondokana na vikwazo kadhaa, lakini bado wanaendelea kukubwa na matatizo  mbali  mbali ikiwemo ukosefu wa huduma.

Hayo yamebainishwa na Mama mwenye  ulemavu  wa viungo ambae  pia ana  watoto 3 wenye  ulemavu  mchanganyiko  mkaazi wa  Konde  wilaya  ya  Micheweni  mkoa wa Kaskazini Pemba  alisema bado anakabiliwa  na changamoto ya  upatikanaji pesa  kwa ajili ya  kununulia  huduma za watoto wake hao.

Akizungumza na mwandisi  wa habari hizi  huko  nyumbani kwake bi Asha Khamis Juma  mkazi  wa  Konde  kiungani mwenye ulemavu  wa viungo alisema bado anakabiliwa na changamoto  kubwa  ya upatikanaji wa  pesa kwa ajili ya  kununulia  Pempasi pamoja na dawa.

‘’Kila siku natumia elfu ishirini [20000] kwa ajili ya kununulia pempasi hivyo nateseka sina uwezo nashinwa nahitaji  msaada jamani’’ alisema mama wa watoto wenye ulemavu.


Alisema kuwa anapatashida katika kuwalea  watoto  wake hao kwani    wote wanaulemavu  mchanganyiko  hawaelewi  lolote huduma zote hadi wafanyiwe ukiangalia na yeye mwenyewe  anaulemavu wa mguu.

‘’Mimi mwenyewe kila baada ya mwaka mmoja na nusu nahitajika nitoe shilingi   laki tano [5000,00] kwa ajili ya kununulia mguu bandia, ukiangalia familia yangu ni masikini haiwezi kuhudumia gharama zangu mimi  pamoja na watoto wangu wenye ulemavu’’ alieleza kwa masikitiko mama mwenye ulemavu.

Alifahamisha kuwa kipindi cha nyuma  Walikwenda  watu wakampa msaada wa gari aina ya Keri kwa ajili ya kuwapelekea watoto Hospital wakati watakapoumwa  lakini haiwezi kuihudumia kwa sasa  kutokana na hali yake.

 ‘’Nilikuja nikapewa msaada wa keri  lakini Hivi ninavyokuambia imelala bandani haina mafuta   na wale wahisani  hawakuja tena’’ alisema mama.


Ali Muhammed Juma ambae ni jirani wa mama huyo  alieleza kuwa  mazingira ya kuwalea  watoto hao ni magumu, hivyo  ipo haja kwa viongozi wa  Serikali, viongozi wa majimbo pambo na wahisani  kumfika na kumuangalia kwa jichpo la huruma mama hoyo ambae amejaliwa na mtihani huo na Allah [s.w].

Mapema  Makamo mwenyekiti wa jumuia  ya Wanawake wenye ulemavu  Hidaya  Mjaka  Ali  aliwataka  wazazi wa watoto wenye ulemavu kuwafichua na kuwaunga  katika jumuiya za watu wenye ulemau  watoto hao  ili wapate kujulikana  jambo ambalo litasaidia kupata fursa mbali mbali za kimaendeleo  wakati  zitakapotokezea.


Nae mratibu  wa  Baraza   la taifa  la  Watu  wenye  ulemavu  Pemba  Mashavu   Juma  Mbarouk  alisema  wamekua  wakiwasaidia  watu  wenye  ulemavu  ambao  wanajishuhulisha  na  harakati  mbali mbali  pamoja na wale wanao jiunga kwenye jumuiya  wakati wanapohitaji  msaada  ijapokua kutafuta hata kwa  wahisani wengine na sio kwa mtu mmoja mmoja.

Kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu cha 12 [1] kinasema ‘’ Watu wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki, bila ya ubaguzi wowote.


 

 

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.