UKOSEFU WA WALIMU MJUMUISHI BADO NI KIKWAZO KWA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU
NA FATMA HAMAD
PEMBA. 17/10/2022
Wazazi wa watoto wenye
ulemavu mkoa wa kaskazini Pemba
wameikumbusha Serikali ya mapinduzi Zanziber
kuboresha miundo mbinu ya wanafunzi wenye ulemavu maskulini ikiwemo
kuweka walimu wanaojua lugha za alama ili watoto wao nawao waweze kupata haki
yao ya elimu.
Kwa upande wake baba
mzazi wa Salum Said Asaa mwenye ulemavu wa macho kutoka Kwale Gongo
alisema kuwa yeye mtoto wake alishindwa kumpeleka skuli kwani anahisi ni
kwenda kupoteza muda tu haoni anachokwenda kukisoma na kukifahamu.
‘’Mimi mtoto wangu alishafika darasa la pili ila nimeshindwa
kumpeleka skuli kwani hakuna mwalimu wa kumfundisha yeye , bali namuacha
ande chekechea tu ili apoteze muda tu mana hata kwenye matokeo yake ni mabaya”,
alieleza mama mzazi wa Salum.
Nae bi Time Bakar Alawi
kutoka Kiuyyu mbuyuni aliitaka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kufanya jitihada
ya kuwasomesha walimu lugha ya alama kwa ajili ya wenye ulemavu ili nawao
waweze kusoma kuanzia msingi hadi vyuo Vikuu.
Mapema mjumbe kutoka
shujuwaza Aziza Alawi Mussa alisema licha ya changa moto hiyo ya uwepo wa uhaba
wa walimu mjumuishi aliwashauri wazazi hao kuwatoa na kuwapeleka skuli waweze
kuchanganyika na wenzao ili wajihisi
kama nawao ni binadamu wenye haki.
Mratibu
wa baraza la taifa la watu wenye ulemavu kisiwani Pemba Mashavu Juma Mabrouk
alisema suala la uhaba wa walimu
mjumuishi bado ni tatizo, hivyo ameishauri
wizara ya elimu kuwapa kipaombele walimu ambao wamesomea fani ya
ukalimani wakati zitakapotokea ajira ili kuona changamoto hiyo imeondoka.
‘’Niishauri
wizara ya elimu wakati itakapotoa nafasi za ajira kuwajiri walimu wengi
waliosomea elimu mjumuishi ili kuona wanafunzi wenye ulemavu nawao wamefaidika
na elimu’’ alieleza Bi Mashavu.
Kaimu
Mratibu Elimu Mjumuisho na Stadi za Maisha ‘EMSM’ Pemba Halima Mohamed Khamis, alisema ujio wa dhana hiyo ndio
iliyokomboa watoto
wenye
ulemavu na wale wenye mahitaji maalum, sasa kupata haki yao ya elimu.
Anasema,
awali watoto wenye ulemavu wa aina mbali mbali, waliachwa bila ya kupatiwa
elimu, kuanzia ngazi ya jamii na serikali kuu.
Lakini
ilipofika mwaka 1991 serikali kupitia wizara ya Elimu ilianzisha madarasa
maalum, kwa ajili ya wanafunzi wenye ulemavu wa akili, ambapo kwa Pemba ni
skuli za Michakaini na Pandani msingi.
Kisha
mwaka 2006, sasa kukazaliwa dhana ya elimu mjumuisho, ambayo ni ule mpango wa
kuwaweka darasa moja katia ya wanafunzi wenye mahitaji na wale wa kawaida.
Anasema,
mpango huo ulianza kwa kusua sua, maana ulikuwa mpya kwa wanafunzi wenye
mahitaji na wale wengine Ambapo hadi sasa, wapo waalimu watano wenye Master, 10
wenye digrii, wakati wenye diploma 20 na 68 ngazi ya cheti wote wana fani ya
Elimu ya Mahitaji Maalum ‘SNE’
‘’Licha
ya takwimu hiyo lakini bado tunashida ya walimu mjumuisho, hivyo tunaiomba
wizara husika kuliweka somo la lazima katika
vyuo ili kila mwalimu akitoka chuoni aweze kusomesha wanafunzi wenye ulemavu
maskulini.
Kaimu
Mratibu alisema wanao wanafunzi wenye uoni hafifu 803, wenye usikivu hafifu
690, wenye ulemavu wa matamshi 405, wenye vichwa vikubwa na vidogo 22.
Kundi
jengine ambalo wanalo katika skuli mbali mbali ni wenye umbikimo 13, mgongo
wazi 7, ulemavu wa akili 111, ulemavu mchanganyiko 113 na ulemavu wa viungo
wanafunzi 91.
Kwa
mujibu wa sheria namba 9 ya mwaka 2006 sheria ya watu wenye ulemavu miaka zaidi ya 40 iliyopita, ilikuwa ni adimu
na ni kichekesho kumkuta mwanafunzi mwenye ulemavu, hasa wa viungo, au wa akili
akiwa ni mmoja kati ya wanafunzi.
Kwa kawaida,
wenye ulemavu na hasa kabla ya kupitishwa kwa sheria yao, nambari 9 ya mwaka
2006, wazazi na walezi wakiishia kuwakomelea majumbani.
Haki ya
elimu, haki ya kucheza, kushiriki na kushirikishwa kwao, ilikuwa ni ndoto ya
mchana, na hawakuonekana kama sehemu ya jamii.
Comments
Post a Comment