MUHALI BADO NI TATIZO.

 

NA FATMA HAMAD PEMBA.

Jamii imekumbushwa kujitokeza kwa wingi mahakamani kutoa  ushahidi kwa kesi za udhalilishaji   jambo ambalo  litasaidia  wahalifu wa makosa hayo kutiwa hatiani na kupata hukumu.

Ukumbusho huo umetolewa na Hakimu wa mahakama aneshughulikia kesi za udhalilishaji  Mkoa wa Kusini Pemba Muumin Ali Juma  wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko ofisini kwake amesema licha  ya Serikali ya Mapinduzi kuweka mikakati mbali mbali ili kuondosha makosa hayo,  ikiwemo uwepo wa mahakama maalumu lakini bado wananchi hawajataka kutoa ushirikiano juu ya mahakama hiyo.

Amesema wananchi waliowengi hawataki kusimama mahakamani kutoa ushahidi na badala yake  huyakalia kitako na kuyafanyia suluhu matukio ya udhalilishaji wakati yanapotokezea katika familia zao  hali ambayo inasababisha kesi nyingi kufutwa mahamani kutokana na kukosa ushahidi.

‘’ kwa kweli  tunakilio kikubwa  Jamii  wenyewe hawajataka kuyaondosha matendo ya udhalilishaji’’ alisema hakimu Muumin.

Alifafanua kuwa kesi nyingi ambazo hazitiwi hatiani na kupata hukumu ni za watoto kuanzia miaka 15 hadi 17.

Alieleza kuwa kila mmoja kwa nafasi yake  aweze kuumwa na vitendo vya udhalilishaji na kuweza kuchukua hatua kwani  kumbuka leo kafanyiwa mtoto wa mwenzako kesho  huenda akafanyiwa wa kwako.

Kwa upandewake  Fatma Rashid Abdala  mwanaharakati wa kupinga masuala ya udhalilishaji kutoka shehia ya Sizini alisema nivyema kwa Serikali kuwachukulia hatua kali za kisheria kwa wale wote wanaokataa kutoa ushahidi ili  iwe muarubaini  wa hilo.

Nae   mratibu wa chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa Fathiya  Mussa  Said amesema wakati umefika kwa wananchi kuacha muhali  juu ya masauala ya udhalilishaji.

Jumla ya mashauri 37  ya udhalilishaji yamepokelewa mahakamani hapo  tokea kuanzishwa mahakama maalumu kwa mwaka huu wa 2022, ambapo mashauri 32  yalirithiwa kutoka mahakama mchanganyiko, mashauri 42 tayari yameshatolewa mamuzi kati ya hayo 7  ndio yaliopata hatia, yaliobakia yalifutwa kutokana na kukosa ushahidi.

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.