JAMII YASHAURIWA KULEA WATOTO KATIKA MALEZI YA PAMOJA

NA FATMA HAMAD, PEMBA

 JAMII imetakiwa kushirikiana katika malezi ya pamoja ili kupatikana kwa kizazi chenye heshma na madili mema.

Ushauri huo umetolewa na Kaimu Mratibu kutoka Ofisi ya mufti Pemba Said Khalfan Issa wakati akizunumza na mwandishi wa habari hizi huko ofisini kwake Chake chake amesema ni vyema jamii kurudisha Mila, Silka na tamaduni za kizanzibar katika kuwalea Vijana.

Alisema zamani mtoto ilikuwa halelewi ni baba na mama pekee, bali kila mmoja alikuwa na nafasi yake, kama vile mwalimu wa madrasa, Shuleni na hata kwa wazazi wengine.

‘’Niombe jamii turudisheni tamaduni zetu za kuwalea watoto wetu katika malezi ya pamoja, ili waepukane na vitendo viou ikiwemo udhalilishaji pamoja na ukahaba,’’alisema.

Alifahamisha kuwa sasahivi kumekuwa kukijitokeza viashiria vingi ambavyo ni hatari kwa watoto,hivyo wakati umefika kurudi katika misingi ya dini inavyoelekeza juu ya malezi,ili kulinda heshma ya wazanzibar.

‘’Kwa kweli hali imekuwa mbaya, kila mmoja hana amani juu ya mtoto wake, hajui ataishi vipi mpaka afike kujielewa, turudini kwenye tamaduni zetu jamani tusiwape uhuru wa kupitiliza vijana wetu,’’alifahamisha.

Asha Omar na Said Juma wananchi kutoka Micheweni walisema kutokuwepo kwa malezi ya pamoja yamechangia kwa kiasi kikubwa suala la mmon’gonyoka wa madili katika jamii.

‘’Zamani mtoto akionekana anafanya kitendo kibaya anakamatwa na kuhukumiwa hapo hapo bila ya kufikishwa kwa wazazi wake, hiyo ilikuwa ikiwafanya watoto kuishi kwa woga, heshma na tabia njema,’’walifahamisha.

Nae mwanaharakati kutoka chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Zanzibar [TAMWA] Pemba Fathiya Mussa Said alisema udhalilishaji bado ni tatizo linaloikumba jamii, hivyo ni vyema jamii kushirikiana katika malezi ili kuwalinda na janga hilo.


 

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.