WANACHI WAHIMIZWA KUYATUNZA NA KUYAENZI MAZINGIRA YA BAHARI

NA FATMA HAMAD, PEMBA

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar,imesema itahakikisha  inachukua  hatua za makusudi za kudhibiti uharibifu wa mazingiara ya baharini  na kuwajengea uwelewa Wananchi juu ya umuhimu wa utunzaji wa mazingira ya baharini.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Ujenzi mawasiliano na Uchukuzi Dokta Khalid Salim  Mohd  wakati akifunga maadhimisho  ya siku ya usafirishaji na usalama wa bahari  huko Gmbani Chake chake   Pemba.

Alisema  binaadamu na viumbe baharini wanategemea bahari katika maisha yao ya kila siku hivyo ni wajibu wa wanachi kulipa umuhimu sualal la utunzaji wa mazingira ya bahari ili kulinda maisha ya viumbe wananchi baharini.

Alisema  pamoja na umuhimu huo bado bahari inakabiliwa na changamoto kubwa ya uharibifu wa mazingira ikiwemo ukataji wa mikoko, utupaji taka ovyo baharini jambo ambalo husababaisha kupoteza maisha ya viumbe baharini pamoja na upandaji wa kina cha maji ya bahari.

Alisema asilimia  70 ya wananchi wa Visiwa vya Zanzibar,wanategea uchumi wa bahari kama vile shughuli za uvuvi wa samaki na ukulima wa zao la Mwani lakini bado jamii haijakuwa na muamko juu ya athari za Mazingira ambazo zinaweza kujitokeza.

‘’Kuna haja kwa Serikali kuwa na Mkakati maalumu katika kudhibiti uharibifu wa mazingira kutokana na baadhi ya wananchi kutotambua athari za mazingira wamekuwa wakitupa machupa ya pastiki na kukata miti ovyo jambo linaloweza kuleta madhara makubwa katika nchi’’alisema Dk,Khalid.


Mapema Mkurugenzi Mkuu ZMA Sheikh Ahmed Mohd Alisema  bahari imekuwa ikileta faida nyingi   kupitia uchumi wa bluu ambapo  wananchi wameweza  kufanya  shughuli nyingi za kujipatia  kipato, na kutoa huku akitoa wito kuendelea kuyatunza  na kuyalinda mazingira ya bahari.

Naye  Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba  Salama Mbarouk Khatibu amesifu juhudi zinzochukuliwa na Wizara ya Ujenzi mawasilino na usafirishaji kwa kuimarisha  huduma za usafiri baharini na Nchi kavu.

Alisema kwa sasa inaonekana Wizara hiyo maeneo mengi ya Pemba,ikiwa katika harakati za ujenzi wa bara bara pamoja na ujenzi wa bandari ya Shumba jambo linatakaloweza kukuza uchumi wa nchi kutokana na kuongezeka kwa shughuli za kibiashara baada ya kukamilika miundombinu hiyo.

Kwa  upande wake Afisa uhusiano kutoka  Chuo Cha Taifa cha  Usafirishaji Tanzania (NiT) Juma Manday  alisema  kuwepo kwa maonyesho hayo kunatoa fursa kwa wananchi kufahamu fursa za ajira  katika fani mbali mbali zinazohusiana na bahari ikiwemo ufundi na ukarabati wa vyombo vya usafiri baharini.

Alisema Serikali ya Awamu wa sita ya Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania,imelekeza nguvu zake miradi ya kimkati katika maswala ya bahari ikiwemo katika utanuzi wa bandari ambapo kuna fusa nyingi hasa kwa Vijana wanaozungukwa na maeneo ya bahari  kutokana nakuwepo kwa  dhana ya uchumi wa bluu hivyo Vijana kama wataweza kupata mafunzo ya fani hizo wataweza kufika mbali.


Awali katika ufungaji wa maadhimisho hayo dk. Khalid alitembelea mabanda mbalimbali ya wadau wa bahari ambapo   kauli mbiu ya mwaka huu inasema ‘’ni miaka 50 ya mapol uwajibikaji  wetu  uwendelee’’.

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.