MTUHUMIWA WA KESI YA ULAWITI AOMBA AACHILIWE HURU


NA FATMA HAMAD, PEMBA

MTUHUMIWA wa kesi ya kunajisi mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 12, ambae ni mwenye ulemavu wa akili anaetambulika kwa jina la Khamis  Salum Ali mkaazi wa Selemu Wete [27], ameiomba mahakama ifute  kesi hiyo, kwani si ya ukeli ni ya uongo,[kusingiziwa].

Mtuhumiwa huyo ameiomba mahakama hiyo mbele ya hakimu wa Mahakama ya kupambana na makosa ya udhalilishaji iliyopo Wete mkoa wa kaskazini Pemba Ali Abdulrahman Ali alisema kuwa siku hiyo aliyosingiziwa kuwa amefanya tukio hilo hakuwepo maeneyo hayo, bali alikuwepo Chasasa kwenye shughuli zake za ujenzi.

‘ ’Mheshimiwa Hakimu mimi sjafanya tukio hilo hizo ni njama tu zilizopangwa na wazazi na wanakijiji wanibambikizie kesi ili ningie hatiani,’’alieleza.

Alisema kuwa ushahidi uliotolewa na Madaktari pamoja na Askari wote ni wa uongo, hivyo ameiomba mahakama ifute kesi hiyo na imuachie huru, kwani hajafanya tukio hilo.

Hakimu  Ali Abdul rahman Ali hakukubaliana na ombi la mtuhumiwa huyo, hivyo alimtaka arudi tena rumande hadi tarehe 21 mwezi huu kwa ajili ya hukumu.

Imedaiwa mahakamani hapo mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo tarehe 5/2/ 2023 majira ya saa 10.00 za jioni huko Selemu wilaya ya Wete mkowa wa Kaskazini Pemba alimuingilia mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 12, mwenye ulemavu wa akili, jambo ambalo ni kosa kisheria, kinyume na kifungu cha 116[1] cha sharia nambari 6/2018, sharia ya Zanzibar.

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.